Na
WyEST
Dodoma

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Franklin Rwezimula leo Machi 25, 2024 ameshiriki kikao na Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mohammed Khamis Abdulla kuhusu namna bora ya kuratibu na kushauri kuhusu matumizi sahihi ya TEHAMA katika utoaji Elimu ikiwa ni mkakati wa kuimarisha ujifunzaji kidijitali



Majadiliano hayo yamehusisha Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari na Mawasiliano na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa yameangazia ubora wa maudhui na vifaa vya kufundishia na miundombinu rafiki ya Kitehama katika Elimu.