SERIKALI KURATIBU ASASI ZA KIRAIA ILI KUIMARISHA HUDUMA ZA ELIMU NA MATUMIZI YA RASILIMALI KWA UWIANO

Serikali kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imetangaza kuanza kuratibu Asasi za Kiraia zinazotekeleza miradi ya elimu nchini, ili kupata taarifa sahihi kuhusu huduma wanazotoa na maeneo yanayonufaika, ili kuimarisha ushirikiano baina ya wadau wa elimu, kuongeza uwazi wa utekelezaji wa shughuli, na kuhakikisha kuwa rasilimali zinatumika kwa ufanisi zaidi katika maeneo yenye uhitaji mkubwa.

Swahili

SERIKALI YAZINDUA MAFUNZO YA LMS NA DARASA JANJA KWA VIONGOZI WA ELIMU NCHINI

Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa kushirikiana na OR-TAMISEMI wameanza kutoa mafunzo ya Ufungamanishaji wa Mfumo wa Usimamizi wa Kujifunza (LMS) na Darasa Janja (Smart Class) kwa viongozi wa mikoa, halmashauri, kata na walimu nchini, yakiwa na lengo la kuimarisha ufundishaji na ujifunzaji kwa njia ya kidigitali.

Swahili

UTEKELEZAJI WA MRADI WA HEET UZINGATIE KUFIKIA MALENGO YA DIRA YA MAENDELEO YA TAIFA 2050 – PROF. NOMBO

Katibu Mkuu wa Wizarau ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo, ametoa wito kwa wadau wa Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi (HEET) kuhakikisha kuwa utekelezaji wa mradi huo unakuwa wa ubunifu, shirikishi, na wenye tija ili kuchangia kikamilifu katika kufanikisha malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, katika sekta ya Elimu, Sayansi na Teknolojia.

Swahili

TANZANIA NA QATAR KUENDELEZA USHIRIKIANO KUIMARISHA SEKTA YA ELIMU

Na

WyEST

Balozi wa Qatar Nchini Tanzania Mheshimiwa Fahad Rashid Al-Marekhi, leo tarehe 7 Agosti 2025, amekutana na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda katika Pfisi za Wizara Jijini Dar ES Salaam

Lengo kuu la ziara hiyo lilikuwa kujadili maeneo ya ushirikiano kati ya Tanzania na Qatar katika Sekta ya Elimu, Sayansi na Teknolojia.

Swahili

TANZANIA NA INDIA KUENDELEZA USHIRIKIANO KATIKA SEKTA YA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo, leo Agosti 07, 2025 Jijini Dodoma amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa India nchini Tanzania, Mhe. Bishwadip Dey ambapo wamejadiliana masuala mbalimbali ya Elimu na namna ya kuimarisha ushirikiano katika nyanja za sayansi na teknolojia.

Swahili

Pages

Subscribe to Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia RSS