BOOST YALETA MAGEUZI YA TEHAMA WALIMU WAJIVUNIA UJUZI MPYA

Mpango wa Kuimarisha na Kuboresha Elimu ya Awali na Msingi (BOOST) umewezesha upatikanaji vifaa vya TEHAMA katika shule teule na vituo vya walimu 400 ili kurahisisha ujifunzaji na ufundishaji kwa njia za Kisasa kutumia teknolojia.



Kupitia mpango huo walimu 600 wa TEHAMA, walimu wakuu 600 na waratibu elimu kata 450 wamepata mafunzo ya matumizi Bora ya vifaa hivyo vya TEHAMA katika kuleta tija kwenye ufundishaji na ujifunzaji.

Swahili

WANAFUNZI WENYE MAHITAJI MAALUM WAKOSHWA NA MIUNDOMBINU YA BOOST

Wanafunzi katika Shule ya Msingi Azimio iliyopo Halmashauri ya Mji wa Makambako mkoani Njombe, wamefurahia ujenzi wa miundombinu bora na jumuishi inayotoa fursa ya elimu kwa wote ikiwemo wanafunzi wenye mahitaji Maalum.



Hawa Njovi, mwanafunzi mwenye ulemavu wa viungo ana malengo ya kuwa daktari wa watoto, amesema miundombinu rafiki inahamasisha ujifunzaji hivyo amewashauri wanafunzi wenye mahitaji Maalum wasikate tamaa.

Swahili

Pages

Subscribe to Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia RSS