MWONGOZO WA KUSHIRIKI KATIKA KAMBI MAALUM YA MAARIFA (BOOTCAMP) KWA AJILI YA MAANDALIZI YA KUJIUNGA NA VYUO VIKUU BORA DUNIANI KATIKA FANI ZA SAYANSI YA DATA, AKILI UNDE, NA SAYANSI SHIRIKISHI KWA MWAKA 2025/2026 (SAMIA SCHOLARSHIP EXTENDED DS/AI+)

Swahili

PROF. DANIEL MUSHI AMEFANYA ZIARA YA KIKAZI KATIKA TUME YA VYUO VIKUU (TCU)

Katika kuimarisha usimamizi wa elimu ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu nchini, Naibu Katibu Mkuu Prof. Daniel Mushi Agosti 29,2025 amefanya ziara ya kikazi katika Tume ya Vyuo Vikuu (TCU) jijini Dar es Salaam.



Ziara hiyo ililenga kuweka Kwa pamoja mikakati ya kuendeleza elimu ya juu ili iwe ya ushindani wa kikanda na kimataifa.

Swahili

PROF MKENDA AKUTANA NA VIONGOZI WA TET NA KAMATI YA TUZO YA UANDISHI BUNIFU YA MWALIMU NYERERE

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Akutana na Viongozi wa TET na Kamati ya Tuzo ya Uandishi Bunifu ya Mwalimu Nyerere



Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, amekutana na kufanya mazungumzo na Baraza la Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) linaloongozwa na Mwenyekiti wake, Prof. Maulid Mwatawala, kujadili uendeshaji wa masuala mbalimbali ya taasisi hiyo.

Swahili

PROF MKENDA TAASISI YA ELIMU YA WATU WAZIMA INATEKELEZA MAJUKUMU MENGI KWA MAENDELEO YA TAIFA

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, amesema kuwa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima imepanua majukumu yake na sasa inatekeleza kazi kubwa zaidi ya suala la watu wazima kujua kusoma, kuandika na kuhesabu.

Akizungumza Agosti 25, 2025 jijini Dar es Salaam, Prof. Mkenda ameeleza kuwa taasisi hiyo imekuwa chachu ya mabadiliko katika elimu jumuishi na elimu bila ukomo kwa watu wote nchini.

Swahili

Pages

Subscribe to Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia RSS