UJUMBE KUTOKA ZANZIBAR WATEMBELEA WIZARA YA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA

Leo, tarehe 19 Agosti 2025, ujumbe kutoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar umetembelea Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu, Prof. Carolyne Nombo.



Lengo kuu la ziara hiyo lilikuwa kujifunza namna Elimu ya Watu Wazima pamoja na Elimu nje ya Mfumo Rasmi inavyotekelezwa Tanzania Bara.

Swahili

SERIKALI KUIMARISHA MATUMIZI YA TEHAMA KATIKA KUFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI

Serikali ya Tanzania imeendelea kutekeleza kwa kasi mageuzi ya elimu, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Sera ya Elimu na Mafunzo ya Mwaka 2014 sambamba na mwelekeo wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050. Mageuzi haya yanalenga kuimarisha ujuzi, sambamba na matumizi ya sayansi na teknolojia katika ufundishaji na ujifunzaji.

Swahili

PROF MUSHI AKUTANA NA MENEJIMENTI YA OUT JIJINI DAR ES SALAAM

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Daniel Mushi, Agosti 15, 2025, amekutana na kufanya mazungumzo na menejimenti ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (Open University of Tanzania - OUT) jijini Dar es Salaam.



Katika kikao hicho, Prof. Mushi alipokea taarifa kuhusu hali ya utoaji elimu chuoni hapo pamoja na maendeleo ya miradi mbalimbali inayoendelea kutekelezwa.

Swahili

10 WAENDA IRELAND SHAHADA ZA UMAHIRI

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Daniel Mushi, leo Agosti 15, 2025, ameshiriki katika semina maalum ya kuwaaga Watanzania 10 waliopata ufadhili wa masomo ya Shahada za umahiri (Masters) kutoka Serikali ya Ireland kupitia Ubalozi wa Ireland nchini Tanzania.



Akizungumza katika hafla hiyo, Prof. Mushi alisema Serikali ya Tanzania inaendelea kufanya juhudi kuhakikisha vijana wanapata fursa za kupata elimu na ujuzi unaohitajika katika ulimwengu sasa.

Swahili

Pages

Subscribe to Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia RSS