HALMASHAURI YA MERU YAJIVUNIA BOOST KUWEZESHA UTEKELEZAJI WA SERA YA ELIMU

Kupitia Program ya BOOST, Halmashauri ya Wilaya ya Meru mkoani Arusha, imepokea jumla ya Sh. Bilioni 2 na milioni 71 ambayo imewezesha ujenzi wa miundombinu mbalimbali ya Elimu ya Awali na Msingi.



Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Zainabu Makwinya kati ya fedha hizo, milioni 332 zinawezesha ujenzi wa Shule ya Msingi kwenye Shule ya Sekondari, ikiwa ni miongoni mwa Shule zinazojengwa nchi nzima kuwezesha utekelezaji wa Sera ya Elimu, kwa kuzingatia Elimu ya lazima sasa ni miaka kumi.

Swahili

DKT. OMAR: ELIMU YA WATU WAZIMA NI SILAHA DHIDI YA UJINGA NA UMASKINI

Mafunzo maalum ya kuwajengea uwezo wawezeshaji wa elimu ya watu wazima, wakiwemo maafisa wa magereza, yamezinduliwa rasmi leo jijini Dodoma, Mafunzo hayo yanaendeshwa na Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW) kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia (WyEST), yakiwa na lengo la kukuza ujuzi na stadi bunifu kupitia mbinu mpya ya RIFLEKTI inayolenga kuimarisha maarifa ya msingi ya KKK (Kusoma, Kuandika na Kuhesabu) pamoja na stadi za maisha.

Swahili

Pages

Subscribe to Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia RSS