PROF. NOMBO ASHIRIKI KIKAO KAZI CHA WENYEVITI WA BODI NA WAKUU WA TAASISI JIJINI ARUSHA
Katibu mkuu wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia Prof. Carolyne Nombo ameshiriki Katika kikao kazi cha Wenyeviti wa Bodi na Watendaji Wakuu wa Taasisi za Umma kinachofanyika kwa siku nne jijini Arusha

ELIMU BULLETIN NA. 42
MDAHALO KUHUSU MAHITAJI YA UJUZI STAHIKI KWA VIJANA BALEHE NJE YA MFUMO RASMI
SERIKALI INAJENGA MIUNDOMBINU YA ELIMU NA KUONGEZA FURSA ZA UFADHILI ELIMU YA JUU - WAZIRI MKENDA
Serikali ya Tanzania inaendelea kuwekeza katika ujenzi wa miundombinu na kuongeza fursa mbalimbali zinazolenga kupata wahitimu mahiri katika nyanja mbalimbali za maendeleo ya Taifa.

Hayo yamebainishwa Agosti 23, 2025 na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf wakati akizungumza katika Shule ya Sekondari Emboreet iliyopo Wilaya ya Simanjiro, ambapo ametaja fursa hizo ikiwemo Samia Skolaship kwa fani za Sayansi, Teknolojia, Uhandisi Elimu Tiba na Hisabati.
PROF. MKENDA AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI YA WASICHANA TUKUTA, SIMANJIRO
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda Agosti 23, 2025 ameweka jiwe la Msingi Mradi wa ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana Tukuta iliyopo Kata ya Terat Wilaya ya Simanjiro mkoani Manyara.

Mradi huo unatekelezwa na Shirika la ECLAT Development Foundation Tanzania chini ya ufadhili wa Shirika la Upendo Foundation kutoka Ujerumani, ukigharimu zaidi ya Sh. Bilioni 4.6, ikiwemo Sh. Milioni 216 thamani ya ardhi iliyotolewa na Kijiji.
VIJANA BALEHE NJE YA MFUMO RASMI WAPEWA WATOA MAONI JUU YA MAHITAJI YA UJUZI
TANZANIA BARA NA ZANZIBAR KUENDELEZA USHIRIKIANO KUBORESHA ELIMU
Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Tanzania Bara kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar wameendelea kuimarisha ushirikiano katika sekta ya elimu, kwa lengo la kuhakikisha mfumo wa elimu unakidhi mahitaji ya soko la ajira la kitaifa, kikanda na kimataifa.
VIJANA BALEHE NJE YA MFUMO RASMI WAPEWA WATOA MAONI JUU YA MAHITAJI YA UJUZI
Katika kutekeleza mageuzi ya elimu nchini, mdahalo maalumu umefanyika ukihusisha vijana balehe waliopo nje ya mfumo rasmi wa elimu, ili kupokea maoni kuhusu aina ya ujuzi wanaopaswa kupewa ili kuwawezesha kujiajiri, kuajiri, na kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi.

