SERIKALI INAJENGA MIUNDOMBINU YA ELIMU NA KUONGEZA FURSA ZA UFADHILI ELIMU YA JUU - WAZIRI MKENDA

Serikali ya Tanzania inaendelea kuwekeza katika ujenzi wa miundombinu na kuongeza fursa mbalimbali zinazolenga kupata wahitimu mahiri katika nyanja mbalimbali za maendeleo ya Taifa.



Hayo yamebainishwa Agosti 23, 2025 na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf wakati akizungumza katika Shule ya Sekondari Emboreet iliyopo Wilaya ya Simanjiro, ambapo ametaja fursa hizo ikiwemo Samia Skolaship kwa fani za Sayansi, Teknolojia, Uhandisi Elimu Tiba na Hisabati.

Swahili

PROF. MKENDA AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI YA WASICHANA TUKUTA, SIMANJIRO

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda Agosti 23, 2025 ameweka jiwe la Msingi Mradi wa ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana Tukuta iliyopo Kata ya Terat Wilaya ya Simanjiro mkoani Manyara.



Mradi huo unatekelezwa na Shirika la ECLAT Development Foundation Tanzania chini ya ufadhili wa Shirika la Upendo Foundation kutoka Ujerumani, ukigharimu zaidi ya Sh. Bilioni 4.6, ikiwemo Sh. Milioni 216 thamani ya ardhi iliyotolewa na Kijiji.

Swahili

Pages

Subscribe to Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia RSS