PROF. NOMBO: VYUO VIKUU NI MSINGI WA MAARIFA NA UBUNIFU KWA TANZANIA
SERIKALI YALENGA KUIFANYA ELIMU YA JUU KUWA YA USHINDANI KIMATAIFA
Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imeeleza kuwa inaendelea kutekeleza ajenda yake ya kuifanya elimu ya juu nchini kuwa ya ushindani katika ngazi ya kimataifa kupitia utekelezaji mpango wa Umataifishaji. (Internationalization).
ELIMU YA JUU NI MSINGI WA MAENDELEO YA TAIFA - PROF. NOMBO
Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo, amesema Vyuo Vikuu nchini ni nguzo muhimu ya maendeleo kwa kuendeleza maarifa kuchochea tafiti na ubunifu, na wataalamu wanaoweza kukabiliana na changamoto za karne ya 21.
SERIKALI YAENDELEA KUIMARISHA UTEKELEZAJI WA SAMIA SKOLASHIPU EXTENDED DS/AI+
Serikali ya Tanzania imeendelea kuonesha dhamira ya kuwezesha vijana wa Kitanzania kupata elimu ya juu katika fani za Sayansi ya Data, Akili Unde na Sayansi Shirikishi kupitia mpango wa Samia Scholarship Extended DS/AI+.
WASHAURI WA WANAFUNZI KATIKA VYUO NI NGUZO KWA MAFANIKIO YA WANAFUNZI KIELEMU
Na WyEST
Zanzibar
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayanai na Tenolojia amesdhughulikia Elimu ya Juu, Sayansi na Teknolojia Prof.Daniel Mushi amesema Washauri wa Wanafunzi katika Vyuo wana nafasi kubwa ya kusaidia wanafunI kufikia malengo yao kielimu.

Amesema hayo Septemba 26 akifunga Mkutano Mkuu wa Mwaka wa 43 wa Chama cha Washauri wa Wanafunzi Tanzania 1984 ( TACOGA1984 ) uliofanyika Maruhubi Kampasi ya Chuo Kikuu SUZA.
TANZANIA KUENDELEA KUIMARISHA MIFUMO YA UTOAJI ELIMU YA JUU
Taasisi ya Sayansi ya Bahari (IMS) ya Chuo Kikuu cha Dar es salaam iliyopo Buyu Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja,
Naibu katibu Mkuu Sayansi na Teknolojia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Daniel Mushi amekutana na Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na mafunzo ya Amali Zanzibar Ndugu Khamis Abdullah Said na kujadiliana kuhusu kuimarisha utoaji Elimu ya Juu kwa kuzingatia mabadiliko ya kisera na uchangamano wa kikanda.
SHULE YA SEKONDARI DKT. SAMIA DODOMA YAKAMILIKA NA KUKABIDHIWA RASMI
Serikali imekabidhiwa rasmi majengo ya Shule ya Sekondari mpya Dkt. Samia iliyopo Iyumbu jijini Dodoma, ambayo imegharimu Shilingi bilioni 17.8.
WIZARA YA ELIMU NA TAMISEMI WAJADILI UTEKELEZAJI WA MRADI WA SEQUIP
Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais – TAMISEMI leo Septemba 26, 2025 wamefanya kikao kazi jijini Dodoma kwa ajili ya kupokea na kujadili utekelezaji wa Mradi wa Secondary Education Quality Improvement Program (SEQUIP).

Katika kikao hicho, pande zote mbili zilikubaliana kuendeleza ushirikiano wa karibu ili kuhakikisha mradi unatekelezwa kwa ufanisi na kuleta matokeo chanya katika sekta ya elimu nchini.
SERIKALI YATENGA ZAIDI YA ASILIMIA 14 KWA ELIMU BORA, JUMUISHI NA ENDELEVU
Serikali kupitia Mpango wa Maendeleo wa Sekta ya Elimu 2025/26-2029/30 imetenga zaidi ya asilimia 14 ya rasilimali za ndani kwa ajili ya miradi ya elimu ili kuendeleza elimu jumuishi, yenye usawa na ubora kwa wote.

