WATAALAM WA LUGHA KUTOKA CUBA WAANZA KUFUNDISHA KIHISPANIA SUA, WAONGEZA NGUVU KATIKA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA
Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kimepokea wataalam wawili wa lugha kutoka nchini Cuba, watakaofundisha lugha ya Kihispania kwa kipindi cha miaka miwili chini ya Idara ya Lugha, katika jitihada za kuendeleza elimu ya kimataifa na kuboresha umahiri wa lugha miongoni mwa wanafunzi.
PROF. NOMBO AUNGANA NA WATANZANIA KATIKA UZIMAJI WA MWENGE WA UHURU MBEYA
Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo, leo Oktoba 14, 2025, ameungana na Watanzania katika Maadhimisho ya Uzimaji wa Mwenge wa Uhuru yaliyofanyika mkoani Mbeya.
ESWATINI WAJA TANZANIA ZIARA YA MAFUNZO YA ULINGANIFU KATIKA SEKTA YA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA
Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imepokea ujumbe wa wataalamu kutoka Falme ya Eswatini ambao wapo katika ziara ya mafunzo ya ulinganifu, inayoratibiwa na taasisi ya Economic Policy and Analysis Research Centre (ESEPARC) kwa kushirikiana na Wizara ya Kazi na Hifadhi ya Jamii (MoLSS) ya Falme ya Eswatini.
SERIKALI YASISITIZA USIMAMIZI MAKINI WA MIRADI YA ELIMU ILI KULINDA RASILIMALI ZA UMMA
Serikali imewataka viongozi wa usimamizi wa miradi ya ujenzi wa miundombinu ya elimu kusimamia kwa ukaribu utekelezaji wa miradi hiyo ili kulinda rasilimali za umma na kuhakikisha thamani ya fedha inaonekana.
MAJALIWA ATOA WITO WA USHIRIKIANO KUJENGA TAIFA LENYE WATU WENYE UJUZI
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Kassim Majaliwa, amesema Serikali itaendelea kuimarisha nguvu kazi yenye ujuzi ili iweze kushindana katika soko la ajira la ndani na kimataifa.

Mhe. Majaliwa amesema hayo 11 Oktoba 2025 jijini Dar es Salaam, wakati akifungua Kongamano la Kumbukizi ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

