PROF. NOMBO AZINDUA MPANGO WA MO-KRRY SCHOLARSHIP KWA AJILI YA KUONGEZA WATAALAMU KATIKA SEKTA YA KILIMO NA CHAKULA

40 wanufaika na ufadhili

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo, amesema kuwa ushirikiano ulioanzishwa kati ya Taasisi ya Mo Dewji, Kampuni ya Kerry Group, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), na Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) utasaidia kuwaunganisha vijana na viwanda wapate ujuzi.

Swahili

FULL SCHOLARSHIP AT GERMAN UNIVERSITY IN CAIRO (GUC) AND GERMAN INTERNATIONAL UNIVERSITY (GIU) IN THE ARAB REPUBLIC OF EGYPT FOR THE ACADEMIC YEAR 2025/2026

The Ministry of Education, Science and Technology is pleased to announce that the German International University (GIU) and the German University in Cairo (GUC) are offering fully funded scholarships to outstanding Tanzanian students.

Swahili

ASILIMIA 20 YA BAJETI KUU HUTENGWA KWA AJILI YA SEKTA YA ELIMU

Naibu Waziri Mkuu ambaye pia ni Waziri wa Nishati, Dk. Dotto Biteko, amesema Serikali imeendelea kuipa kipaumbele sekta ya elimu kwa kutenga takribani asilimia 20 ya Bajeti Kuu kila mwaka kwa ajili ya sekta hiyo.



Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano wa wadau wa elimu ulioandaliwa na Mtandao wa Elimu Tanzania (TEN/MET) jijini Dar es Salaam Septemba 24,2025 Dk. Biteko amesema hatua hiyo imeifanya Tanzania kuwa mfano wa kuigwa barani Afrika.

Swahili

PROF. CAROLYNE NOMBO NA BI. SUZZANE NDOMBA WAJADILI MIKAKATI YA KUIMARISHA UJUZI WA VIJANA KWA AJIRA

Katika kuhakikisha kuwa mafunzo ya darasani yanaendana na mahitaji halisi ya soko la ajira, Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo, amekutana na Afisa Mtendaji Mkuu wa Chama cha Waajiri Tanzania (ATE), Bi. Suzzane Ndomba, kwa mazungumzo ya kina kuhusu namna ya kuwawezesha vijana wanaohitimu vyuoni kupata mafunzo ya vitendo sehemu za kazi.

Swahili

PROF. CAROLYNE NOMBO: MAGEUZI YA ELIMU YANAHITAJI UWEKEZAJI WA RASILIMALI FEDHA NA WATU

Serikali imesisitiza kuwa maboresho makubwa yanayoendelea katika sekta ya elimu yanahitaji uwekezaji wa kutosha wa rasilimali fedha na watu ili utekelezaji wake uwe wa ufanisi na wenye matokeo chanya.



Kauli hiyo imetolewa Jijini Dar es Salaam, Septemba 24, 2025 na Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo, wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Kimataifa wa Kujadili Ubora na uwekezaji katika sekta ya Elimu ulioandaliwa na Mtandao wa Elimu Tanzania (TEN/MET).

Swahili

TANZANIA YAKUWA MWENYEJI WA MKUTANO WA 20 WA KISEKTA WA MAWAZIRI WA ELIMU NA UTAMADUNI

Tanzania imekuwa Mwenyeji wa Mkutano wa 20 wa Kisekta wa Mawaziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Utamaduni na Michezo ambao umefanyika Jijini Dar es Salaam Septemba 23, 2025



Mkutano huo ambao Mwenyekiti wake ni Waziri wa Elimu kutoka Kenya umehudhuriwa na wajumbe kutoka nchi wanachama ambapo ujumbe wa Tanzania umeongozwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Aftika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Dennis Londo

Swahili

PROF. NOMBO: KITUO CHA UMAHIRI MUHAS NI NGUZO YA KUINUA UTAALAMU WA AFYA NCHINI

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo, amezindua Kamati Tendaji ya Kituo cha Umahiri cha Magonjwa ya Moyo na Mishipa ya Damu kilichopo Mloganzila, kinachomilikiwa na Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS), ambapo amesisitiza umuhimu wa kuvilinda na kuvitunza vifaa vya kisasa vilivyopo kituoni hapo ili viendelee kutoa mchango mkubwa kwa maendeleo ya sekta ya afya.

Swahili

Pages

Subscribe to Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia RSS