WIZARA YA ELIMU NA ELIMU MATOKEO WAZUNGUMZIA MAGEUZI YA ELIMU
Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo, Januari 26, 2026 jijini Dodoma, amekutana na kufanya mazungumzo na Mtendaji Mkuu (CEO) wa Taasisi ya Elimu Matokeo, Bi. Rakshita Vaya, kwa lengo la kujadili maboresho ya mfumo wa elimu nchini.

Taasisi ya Elimu Matokeo inalenga kubadilisha mfumo wa elimu kwa kutoa programu bora, jumuishi na zinazopatikana kwa urahisi ili kukidhi mahitaji ya wanafunzi wa ngazi mbalimbali pamoja na jamii kwa ujumla.



