RAIS SAMIA ATOA MAELEKEZO YA UTEKELEZAJI WA MKAKATI WA ELIMU
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, ametoa maelekezo kwa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI na wizara nyingine zinazoshughulika na elimu kuhakikisha utekelezaji kamili wa Mpango Mkakati wa Kisayansi wa Kujenga Umahiri Kusoma, Kuandika na Kuhesabu (KKK).
SERIKALI YAZINDUA MPANGO WA KISAYANSI WA KKK, KUTEKELEZWA HADI 2030
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, amesema serikali imeandaa mkakati wa Kisayansi wa kuboresha kitaifa wa kuimarisha umahiri katika kuandika, kusoma na kuhesabu ikiwa ni utekelezaji wa ahadi za Mhe Rais kwa Watanzania.
UMAHIRI WA KKK: MSINGI WA MAFANIKIO YA ELIMU
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila amesema kumudu lugha na kuimarisha ujuzi wa Kusoma, Kuandika na Kuhesabu kutawawezesha wanafunzi kuelewa vyema kila wanachofundishwa na hivyo kufanikisha malengo ya elimu.
SERIKALI YAZINDUA MKAKATI WA KISAYANSI WA KUSOMA, KUANDIKA NA KUHESABU KWA WATOTO WA TANZANIA
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imejipanga kuimarisha umahiri wa kusoma, kuandika na kuhesabu kwa watoto wa elimu ya awali na wanafunzi wa darasa la kwanza na la pili. Kupitia Mkakati wa Kisayansi, hatua hii inalenga kuweka msingi thabiti wa maarifa na ujuzi wa msingi, ili kuhakikisha kila mtoto anapata nafasi ya kujengewa uwezo wa kitaaluma na kiujuzi mapema.
UZINDUZI WA MPANGO MKAKATI WA KISAYANSI WA KUJENGA UMAHIRI
WAZIRI MKENDA AWAALIKA WATANZANIA KWENYE UZINDUZI WA MKAKATI WA KISAYANSI WA ELIMU MSINGI
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Prof. Carolyne Nombo, tarehe 28 Januari 2026 kupitia Televisheni ya Taifa (TBC1), wamewaalika Watanzania kushiriki katika uzinduzi wa Mkakati wa Kisayansi wa Kujenga Umahiri wa Kusoma, Kuandika na Kuhesabu kwa watoto wa Elimu ya Awali na wanafunzi wa Darasa la Kwanza na la Pili.
SERIKALI YABORESHA MFUMO WA MIKOPO YA ELIMU YA JUU KUPITIA TEKNOLOJIA YA AKILI BANDIA
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Daniel Mushi, amesema Serikali kupitia wizara hiyo inaendelea kusimamia kwa karibu mapitio ya muundo na mfumo wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), kwa lengo la kuboresha mifumo ya upangaji na utoaji wa mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu.

PROF. NOMBO AKUTANA NA MKURUGENZI WA FCDO KUJADILI USHIRIKIANO WA ELIMU
Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo, tarehe 27 Januari 2026, amekutana na Ms Anna Wilson, Mkurugenzi wa Maendeleo ya Rasilimali Watu kutoka Ofisi ya Mambo ya Nje, Jumuiya ya Madola na Maendeleo ya Uingereza (FCDO).

Lengo la kikao hicho kilikuwa ni kujitambulisha pamoja na kumpitisha mgeni huyo katika majukumu na kazi mbalimbali zinazotekelezwa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia katika kuendeleza sekta ya elimu nchini.
NAIBU KATIBU MKUU PROF. DANIEL MUSHI: UPANDAJI MITI NI ALAMA YA KUDUMU KWA UHIFADHI WA MAZINGIRA
Naibu Katibu Mkuu, Prof. Daniel Mushi, amesema kuwa zoezi la upandaji miti lililofanyika kwa heshima ya siku ya kuzaliwa ya Rais ni hatua ya kihistoria ya kulinda mazingira na kuacha kumbukumbu ya kudumu kwa vizazi vijavyo.

