SERIKALI YAZINDUA MPANGO WA KUKUZA UJUZI NA AJIRA KWA VIJANA

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, amesema kuwa uzinduzi wa Mpango wa Kitaifa wenye lengo la Kukuza Ujuzi na Ajira ni utekelezaji wa ahadi ya Rais Samia Suluhu Hassan aliyoitoa wakati wa Kampeni za uchaguzi kwa mwaka 2025 kwamba ndani ya siku 100 endapo atachaguliwa na kuapishwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Serikali ingeandaa na kuzindua Mpango wa kukuza ujuzi na uwezo wa kuajirika kwa vijana, na sasa ahadi hiyo imetimia kabla ya muda uliowekwa.

Swahili

KAMATI YA BUNGE YAPONGEZA MAGEUZI YA ELIMU, YAAHIDI USHIRIKIANO NA WIZARA

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Michezo na Utamaduni, Mhe. Husna Sekiboko, leo Februari 9, 2026 katika uzinduzi wa Mpango wa pamoja wa Ushirikiano kati ya Taasisi za Elimu na Viwanda unaofanyika Jijini Dar es Salaam ameipongeza Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa mageuzi makubwa yaliyofanyika kwa muda mfupi wa kuhakikisha vijana wanapata ujuzi.

Swahili

WALIMU 1,055 WANUFAIKA NA VIFAA MAALUMU VYA KIDIGITALI VYENYE THAMANI YA BILIONI 5.3

Serikali imesema itaendea kuweka  mkazo katika kuimarisha maslahi, ushiriki na mazingira ya kazi kwa walimu wanawake na walimu wenye ulemavu ikiwa ni sehemu ya juhudi za kujenga mfumo jumuishi wa elimu unaotoa fursa sawa kwa wote.



Hayo yamesemwa jijini Dodoma Februari 6, 2026 na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Wanu Hafidh Ameir wakati wa ufunguzi wa kikao cha Wawakilishi wa Walimu Wanawake na Walimu wenye ulemavu kutoka mikoa yote ya Tanzania Bara.

Swahili

Pages

Subscribe to Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia RSS