TUHAKIKISHE KAMPASI MPYA ZA VYUO VIKUU ZINATOA MAFUNZO YA UJUZI
Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imesisitiza kuwa Vyuo Vikuu vinavyojenga kampasi mpya katika maeneo mbalimbali nchini kuhakikisha kampasi hizo zinajikita katika kutoa mafunzo ya ujuzi (Amali).

Agizo hilo limetolewa jijini Dodoma na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, wakati wa kikao kazi cha kimkakati kati ya Wizara na Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya Wizara.
VIJANA KUANDALIWA KUSHIRIKI KIKAMILIFU KATIKA UZALISHAJI WA TAIFA - MHE. WANU HAFIDH
Wizara na Taasisi tunajipanga kimkakati kufikia malengo mapana ya Taifa ya kuzalisha nguvu kazi yenye ujuzi utakao wezesha vijana kupata kushiriki kikamilifu katika shughuli za uzalishaji na kuchangia maendeleo ya Taifa." Mhe . Wanu Hafidh Ameir Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia.

VIONGOZI WA ELIMU WAWEKA MIKAKATI KUFIKIA MALENGO YA DIRA 2050
Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Carolyne Nombo ameeleza kuwa Wizara na Taasisi zilizo chini yake zimekutana jijini Dodoma Januari 20, 2026 kuangalia utekelezaji wa Malengo 2025/26 na kuweka mikakati ya pamoja ya kuwezesha ufikiaji malengo ya Dira 2050 katika sekta za Elimu, Sayansi na Teknolojia.

