SHEIKH MKUU WA TANZANIA APONGEZA LALJI FOUNDATION KWA KUSAIDIA ELIMU YA WATOTO WASIOJIWEZA
Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Sheikh Dkt. Abubakar Zuber Ali Mbwana, ameipongeza Taasisi ya Lalji Foundation kwa jitihada za kutoa misaada kwa watoto yatima na wasiojiweza, akisisitiza kuwa ni matendo yenye thawabu kubwa mbele ya Mwenyezi Mungu.

Kiongozi huyo ametoa pongezi hizo Januari 10, 2026 jijini Dar es Salaam katika hafla ya ugawaji wa vifaa mbalimbali kwa wanafunzi kutoka vituo vya kulea watoto yatima, chini ya ufadhili taasisi hiyo.
WAZIRI MKENDA AIPONGEZA LALJI FOUNDATION KWA MCHANGO WA KUHAKIKISHA WATOTO WANAPATA ELIMU BORA
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, amesema Serikali inaendelea kuunga mkono juhudi za Taasisi ya Lalji Foundation katika kuimarisha sekta ya elimu na maendeleo ya kijamii, hususan katika kuhakikisha watoto wanapata elimu bora na jumuishi.

