SERIKALI INAENDELEA KUWEKEZA KATIKA ELIMU YA WATU WAZIMA - PROF. MUSHI
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Daniel Mushi, amesema Serikali inaendelea kuwekeza katika kukuza elimu jumuishi, mbadala na endelevu, hususan kwa wananchi waliokosa fursa ya elimu katika mfumo rasmi.

