PROF. MKENDA AZINDUA UGAWAJI VIFAA SAIDIZI VYA KIDIGITALI KWA WALIMU WENYE ULEMAVU VYENYE THAMANI YA SH. BILIONI 5.3

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Prof. Adolf Mkenda amezindua ugawaji wa vifaa vya kielimu na saidizi kwa walimu, wakufunzi na walimu tarajali wenye ulemavu vyenye thamani ya Sh. Bilioni 5.3.



Uzinduzi huo umefanyika Januari 05, 2026 jijini Dodoma, ambapo Waziri Mkenda amesema kuwa Serikali inaendelea na utekelezaji wa sera na maboresho ya mitaala, na kwamba jitihada za uwekezaji zimewezesha wanafunzi wenye mahitaji maalum kupata elimu bora.

Swahili

NM-AIST YAWEZESHA VIJANA KUSOMA NJE YA NCHI, YAONGEZA UWEKEZAJI WA MIUNDOMBINU

Makamu Mkuu wa Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela (NM-AIST), Prof. Maulilio Kipanyula, amesema kuwa mpaka sasa taasisi hiyo imewawezesha vijana kupata udahili katika vyuo mbalimbali duniani.



Ameeleza kuwa wanafunzi 16 wamepata nafasi nchini Afrika Kusini, 29 wamepata nafasi nchini Ireland, na watano wako katika hatua ya mahojiano ya ana kwa ana kwa ajili ya kupata udahili.

Swahili

SAMIA SKOLASHIPU DS/AI+ KUONGEZA WATAALAMU WA TEKNOLOJIA NA TAKWIMU

Serikali kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia inatekeleza mpango maalumu wa kujenga uwezo wa nchi katika teknolojia za Takwimu, Akili Unde na Sayansi Shirikishi (DS/AI+) kupitia Programu ya Samia Scholarship Extended ambapo vijana 50 wanajiandaa kupelekwa nje ya nchi kusoma shahada za kwanza katika fani hizo, kuiwezesha Tanzania kutekeleza mageuzi ya kidijitali na kuzalisha ajira mpya.

Swahili

Pages

Subscribe to Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia RSS