MAGEUZI YA ELIMU YATAWEZESHA VIJANA KUJENGA TAIFA LENYE NGUVU NA UCHUMI ENDELEVU
Serikali imeendelea kufanya uwekezaji mkubwa katika ujenzi na uboreshaji wa miundombinu ya elimu pamoja na kuongeza fursa za masomo katika ngazi mbalimbali. Miongoni mwa hatua hizo ni kuongezeka kwa bajeti ya mikopo ya elimu ya juu kutoka Sh. bilioni 464 mwaka 2020/21 hadi Sh. bilioni 926.7 mwaka 2025/26.

