Serikali Inaendelea na Jitihada za kuondoa Changamoto ya Mdondoko wa Wanafunzi

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Carolyne Nombo amesema kuwa serikali inaendelea na jitihada za kuondoa changamoto ya mdondoko wa wanafunzi



Prof. Nombo amesema hayo Machi 15, 2024 Jijini Dar es Salaam wakati Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo ilipotembelea Baraza hilo ambapo amesema sehemu ya jitihada hizo ni pamoja na ujenzi wa shule za kata ili kuwapunguzia wanafunzi kutembea mwendo mrefu.

Swahili

Ruzuku ya Mitihani Iliyokuwa Imepangwa 83% Imeshatolewa ambapo Imewezesha Kutekeleza Malengo ya Taasisi - Dkt. Said Mohamed

Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Tanzania Dkt. Said Mohamed amesema kati ya ruzuku ya mitihani iliyokuwa imepangwa 83% imeshatolewa mpaka kufikia Mwezi Februari 2024 ambapo imewezesha kutekeleza malengo ya Taasisi.



Akizungumza Machi 15, 2024 Jijini Dar es Salaam wakati Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo ilipotembelea Baraza hilo kujionea namna fedha zilizotengwa katika Mwaka wa Fedha wa 2023/24 zilivyotumika.

Swahili

Nyaraka za Usimamizi wa Maafa zitakuwa ni za kitaifa na wadau waliopewa majukumu katika nyanja za biolojia, kemikali na nyuklia watazitumia kwa kuzingatia mahitaji ya Taasisi zao.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda amesema Nyaraka za Usimamizi wa Maafa zitakuwa ni za kitaifa na hivyo taasisi na wizara mbalimbali na wadau waliopewa majukumu katika nyanja za biolojia, kemikali na nyuklia watazitumia kwa kuzingatia mahitaji ya Taasisi zao.

Swahili

Mhe. Kassim Majaliwa amezindua Nyaraka za Usimamizi wa Maafa na kushuhudia zoezi la utayari wa kukabiliana na dharura za Kikemikali na Mionzi

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Machi 14, 2024 jijini Dar es Salam amezindua Nyaraka za Usimamizi wa Maafa na kushuhudia zoezi la utayari wa kukabiliana na dharura za Kikemikali na Mionzi

Swahili

Pages

Subscribe to Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia RSS