Walimu ndio Kitovu cha Mafanikio ya Mitaala Iliyoboreshwa

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Carolyne Nombo amesema kuwa, ili kuwe na mafanikio katika utekelezaji wa Sera ya Elimu na Mitaala lazima kuwekeza katika kada ya Ualimu.



Prof. Nombo amesema hayo wakati akifungua kikao kazi kati ya Serikali, Shirika lisilo la Kiserikali la Mastercard Foundation na Wadau wa Sekta ya Elimu kwa lengo la kujadili namna ya kuimarisha kada ya ualimu kilichofanyika Machi 18, 2024 Jijini Dar es Salaam.

Swahili

Serikali imeanza ujenzi wa vyuo vya Ufundi na Ufundi Stadi (VETA) katika Wilaya 64 ambazo hazikuwa na vyuo hivyo

Serikali imeanza ujenzi wa vyuo vya Ufundi na Ufundi Stadi (VETA) katika Wilaya 64 ambazo hazikuwa na vyuo hivyo pamoja na Chuo cha Mkoa wa Songwe.


Haya yameelezwa na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Omari Kipanga Machi 16, 2024 Jijini Dar es Salaam wakati Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo ilipotembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa Chuo cha ufundi na Ufundi Stadi cha wilaya ya Kinondoni kinachojengwa Mabwepande.

Swahili

Chumba cha Kidigitali (Smart Class) cha Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) chaikosha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu

Chumba cha Kidigitali (Smart Class) cha Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) chaikosha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo



Kamati hiyo ilifika katika Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) kwa ajili ya kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa na taasisi hiyo kupitia bajeti ya Mwaka wa Fedha 2023/24 iliyopitishwa na Bunge.

Swahili

Baadhi ya wanafunzi wakiwaonyesha Wabunge wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu namna wanavyoingiza Sauti kupitia studio zilizopo katika TET

Baadhi ya wanafunzi wakiwaonyesha Wabunge wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo namna wanavyoingiza Sauti kupitia studio zilizopo katika Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) katika vipindi vinavyofundishwa kupitia redio. Vipindi hivyo hutumika kufundisha kupitia redio na Televisheni

Swahili

Kazi ya Uandishi na Uchapaji wa Mitaala, Mihtasari, Vitabu vya Kiada na Viongozi vya Mwalimu kwa Darasa la Kwanza, Tatu na kidato cha Nne Mkondo wa Amali Imekamilika - Dkt. Aneth Komba

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) Dkt. Aneth Komba amesema kazi ya uandishi na uchapaji wa mitaala, mihtasari, vitabu vya kiada na Viongozi vya Mwalimu kwa Darasa la kwanza, tatu na kidato cha nne mkondo wa Amali imekamilika.

Swahili

Pages

Subscribe to Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia RSS