WyEST, TAMISEMI na Benki ya Dunia wamekutana na kufanya majadiliano na tathimini ya utekelezaji wa Mradi wa BOOST

Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Ofisi ya Rais TAMISEMI na Benki ya Dunia Machi 26, 2024 Jijini Dar es Salaam wamekutana na kufanya majadiliano na tathimini ya utekelezaji wa Mradi wa BOOST



Majadliano hayo yanafanyika mara baada ya kufanya ziara ya pamoja ya kujionea hatua za utekelezaji wa mradi huo katika maeneo mbalimbali nchini

Swahili

Chuo Kikuu Ardhi chaanza kwa kasi utekelezaji wa ujenzi wa majengo nane unaofadhiliwa na Mradi wa HEET

Majengo hayo ni pamoja na madarasa, vyumba vya Mihadhara, maabara, studio na ofisi za walimu ambayo yamefikia asilimia 39 ya ujenzi.



Akiongea Machi 25, 2024 Jijini Dar es Salaam Naobu Katibu Mkuu Prof. James Mdoe amesema ameridhishwa na kasi na hatua iliyofikiwa kwa kuwa ujenzi wa majengo hayo ulianza Mwezi wa Agosti 2023 na kuwataka wakandarasi kuhakikisha wanakamilisha ujenzi huo kwa muda uliopangwa na kwa ubora.

Swahili

Vijana wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wametakiwa kuwa mstari wa mbele kushiriki katika Mustakabali wa Maendeleo ya Jumuiya hiyo

Wito huo umetolewa Machi 25, 2024 Jijini Dar es Salaam na Naibu Katibu Mkuu Prof. James Mdoe akifungua Mdahalo wa nane wa Wanafunzi wa Vyuo Vikuu vya nchi za Afrika Mashariki unaofanyika katika Chuo Kikuu Ardhi Kampasi Kuu, mada kuu ya mdahalo ikiwa utangamano, amani na demokrasia katika nchi katika nchi hizo.

Swahili

Wizara ya Elimu, Habari na TAMISEMI waweka Mikakati Matumizi ya TEHAMA katika Elimu

Na
WyEST
Dodoma

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Franklin Rwezimula leo Machi 25, 2024 ameshiriki kikao na Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mohammed Khamis Abdulla kuhusu namna bora ya kuratibu na kushauri kuhusu matumizi sahihi ya TEHAMA katika utoaji Elimu ikiwa ni mkakati wa kuimarisha ujifunzaji kidijitali

Swahili

Prof. James Mdoe amewasili Chuo Kikuu Ardhi jijini Dar es Salaam tayari kufungua Mdahalo wa Nane wa Wanafunzi wa Vyuo Vikuu vya Afrika Mashariki

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. James Mdoe amewasili Chuo Kikuu Ardhi jijini Dar es Salaam tayari kufungua Mdahalo wa Nane wa Wanafunzi wa Vyuo Vikuu vya Afrika Mashariki kuhusu uhusiano wa Kikanda.



Mdahalo huo unaofanyika Machi 25, 2024 umeandaliwa na Jumuiya ya Afrika Mashariki na kufadhiliwa na Umoja wa Ulaya (European Union)

Swahili

Pages

Subscribe to Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia RSS