Prof. Nombo amekutana na waratibu wa Mradi wa Ushirika wa kimataifa wa kusaidia Maendeleo ya Elimu Global Partnership in Education (GPE) na ubalozi wa Sweden

Tarehe 16 April, 2024 Jijini Dodoma, Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Caloryne Nombo amekutana na kufanya mazungumzo na waratibu wa Mradi wa Ushirika wa kimataifa wa kusaidia Maendeleo ya Elimu Global Partnership in Education (GPE) na ubalozi wa Sweden.



GPE ni mfadhili wa miradi mbalimbali ya Elimu nchini ambapo hivi karibuni Serikali ya Tanzania imezindua mradi mwingine mkubwa utakaofadhili na kuboresha kada ya Ualimu nchini.

Swahili

Wizara inaendesha mafunzo ya kuwajengea uwezo Wathibiti Ubora wa Shule

Katika kuendelea kuwajengea uwezo watekelezaji mbalimbali wa Sera ya Elimu na Mafunzo ya Mwaka 2014 Toleo la 2023, Wizara inaendesha mafunzo ya kuwajengea uwezo Wathibiti Ubora wa Shule.



Mafunzo hayo yaliyoanza Aprili 15, 2024 katika Chuo cha Ualimu Morogoro yana lengo la kuwawezesha wathibiti hao kufahamu juu ya mwongozo wa upimaji shirikishi wa matokeo ya ujifunzaji kulingana na kitita cha ubora wa ufundishaji wa elimu ya awali.

Swahili

Adolf Mkenda, Omari Kipanga, Prof. Carolyne Nombo, Prof. James Mdoe na Viongozi wengine wa WyEST wameshiriki usiku wa hafla ya Utoaji Tuzo ya Taifa ya Mwalimu Nyerere

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda, Naibu Waziri Naibu Waziri Omari Kipanga, Katibu Mkuu Prof. Carolyne Nombo, Naibu Katibu Mkuu Prof. James Mdoe na Viongozi wengine wa Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia wameshiriki usiku wa hafla ya Utoaji Tuzo ya Taifa ya Mwalimu Nyerere ya Uandishi Bunifu 2025 zinazofanyika Aprili 13, 2024 Jijini Dar es Salaam

Swahili

Washindi wa Kwanza wa Tuzo ya Taifa ya Mwalimu Nyerere ya Uandishi Bunifu 2024

Washindi wa Kwanza wa Tuzo ya Taifa ya Mwalimu Nyerere ya Uandishi Bunifu 2024 katika nyanja ya Riwaya, Shairi na Hadithi za watoto



Washindi hawa wametangazwa Aprili 13, 2024 Jijini Dar es Salaam katika hafla ya utoaji tuzo hizo ambapo Mgeni Rasmi alikuwa Prof. Abdurazack Gurnah Mshindi wa Tuzo ya Nobel katika Fasihi Mwaka 2021.

Swahili

Pages

Subscribe to Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia RSS