MRADI WA HEET KUIWEZESHA TAASISI YA SAYANSI ZA BAHARI KUONGEZA UDAHILI NA PROGRAMU ZA MAFUNZO

Timu ya Benki ya Dunia Oktoba 28, 2024 imeendelea na ziara yake ya kukagua Miradi inayotekelezwa na Taasisi za Elimu ya Juu kupitia Mradi wa Elimu ya Juu kwa Maendeleo ya Kiuchumi (HEET) unaofadhiliwa na benki hiyo.



Akitoa taarifa ya utekelezaji wa Mradi huo katika Kampasi ya Buyu, Mratibu Msaidizi Dkt. Libereta Haule amesema kuwa mradi umewezesha kuongeza udahili wa wanafunzi katika kampasi hiyo ya awali kutoka 139 hadi kufikia 278.

Swahili

WATEKELEZAJI MRADI WA HEET WAKUTANA KUSUKA MIKAKATI YA UTEKELEZAJI

Watekelezaji wa Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi (HEET) leo Oktoba 22, 2024 wamekutana Mkoani Mwanza kufanya mapitio ya utekelezaji wa mradi (Midterm Hb Review) kutathimini mafanikio, kubaini changamoto na maboresho yanayotakiwa kufanyika ili kuongeza ufanisi katika utekelezaji ili kufikia katika kuleta mapinduzi ya kiuchumi kulingana na malengo ya mradi.

Swahili

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni, na Michezo imepokea taarifa ya Utekelezaji wa Tahasusi mpya za kidato cha tano

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni, na Michezo imeendelea na vikao vya kupokea taarifa kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia



Leo Oktoba 21, 2024 jijini Dodoma Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imewasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Tahasusi mpya za kidato cha tano na ushirikishwaji wa Wadau kwenye uandaaji wa tahasusi hizo

Swahili

Pages

Subscribe to Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia RSS