USIKOSE FUATILIA NI SAA 3.30 USIKU TBC. ELIMU UJUZI NDIO MPANGO MZIMA
KIPINDI MAALUM - ZIARA YA PROF. MKENDA MKOANI NJOMBE
SIMULIZI YA KIJANA ALIYEPETA UFADHILI WA MRADI WA EASTRIP NA SASA NI MWALIMU NA FUNDI WA NDEGE
MRADI WA EASTRIP WAWEZESHA NIT KUTOA WATAALAM WABOBEZI WA ANGA NA USAFIRISHAJI AFRIKA MASHARIKI
TUPO MSTARI WA MBELE KUCHANGIA SEKTA YA ELIMU - MRATIBU TENMET.
AGENDA YETU NI KUWEKEZA KWENYE ELIMU UJUZI - PROF. MKENDA
AGENDA YETU NI KUWEKEZA KWENYE ELIMU UJUZI - PROF. MKENDA
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda amewataka wadau kuiunga mkono Serikali kutekeleza mageuzi ya elimu nchini ikiwa ni pamoja na kuwekeza katika elimu ujuzi inayolenga kuliwezesha taifa kuwa na rasilimali watu yenye umahiri katika sekta mbalimbali.
Mradi wa EASTRIP waongeza Udahili wa Wanafunzi kwa kasi DIT
NA WyEST
Dar es Salaam
Utekelezaji wa Mradi wa Kujenga Ujuzi na Ushirikiano Afrika Mashariki (EASTRIP) umeiwezesha Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (,DIT) kuongeza udahili wa wanafunzi kutokana 800 hadi kufikia 1500.
Akizungumza Novemba 13, 2024 Jijini Dar es Salaam wakati wa ziara ya Timu kutoka Benki ya Dunia na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia iliyokuwa ikikagua maendeleo ya Mradi huo, Mratibu wa Mradi Dkt. Joseph Matiku amesema kuwa tangu kuanza kwa mradi huo Mwaka 2018 Taasisi imeongeza udahili maradufu.

