WALIMU WAKUU 17,793 WAWEZESHWA MAFUNZO YA UONGOZI NA USIMAMIZI WA SHULE
Bi. Anna Mhere amewatembelea washiriki wa mafunzo ya Uongozi na Usimamizi wa Shule
Mkaguzi wa Ndani Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Tekonolojia Bi. Anna Mhere leo Novemba, 2024 amewatembelea washiriki wa mafunzo ya Uongozi na Usimamizi wa Shule yanayowahusisha Walimu Wakuu katika kituo cha mafunzo cha Kashato-TRC kilichopo Manispaa ya Mpanda mkoani Katavi.
Dkt. Hussein Ally Mwinyi kuzindua Ofisi na Maabara ya Teknolojia ya Nyuklia Zanzibar
Hayo yamesemwa leo Nov, 07, 2024 Jijini Dodoma na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda ambapo Mkenda amesema kuwa miundombinu hii ni ya kisasa na inaendana na Azma ya Rais wa Jamhuri ya Muumgano wa Tanzania Dkt Samia Saluhu Hasana ya kutaka huduma muhimu ya uthibiti wa matumizi ya Nyuklia ipelekwe karibu na Wananchi.
RAIS SAMIA KUZINDUA MFUKO WA KUENDELEZA KAZI ZA WABUNIFU
Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuzindua Mfuko wa Mikopo wa kusaidia Ubidhaishaji na Ubiasharishaji wa ubunifu na teknolojia zinazobuniwa na vijana wa Kitanzania.
WALIMU WAKUU 17,793 WAWEZESHWA MAFUNZO YA UONGOZI NA USIMAMIZI WA SHULE KUPITIA MRADI WA BOOST
Serikali kupitia Mradi wa Kuboresha Elimu ya Awali na Msingi (BOOST) imewezesha mafunzo Walimu Wakuu 17,793 katika Mikoa 26 ya Tanzania Bara kuhusu uongozi na usimamizi wa Shule.

Hayo yamesemwa Novemba 06, 2024 mkoani Katavi na Mkurugenzi wa Elimu ya Awali na Msingi Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Abdul Maulid akizungumza katika halfa ya kuhitisha mafunzo hayo kitaifa ambapo amewataka walimu kusimamia ustawi na usalama wa wanafunzi shuleni.
ELIMU YA LAZIMA SASA MPAKA KIDATO CHA NNE
Kufuatia Mapitio ya Sera ya Elimu ya Elimu ya Mwaka 2014 na mabadiliko ya Mitaala Elimu Msingi hivi sasa Elimu ya lazima ni miaka 10.

Amesema wanafunzi wakitoka Elimu ya Awali ya mwaka mmoja, kuanzia sasa Elimu ya Msingi nj miaka 6, Elimu ya Sekondari ya chini miaka 4.
Prof. Adolf Mkenda amekutana na Mkurugenzi Mtendaji wa COSTECH Dr Amos Nungu
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda leo hii Novemba 05, 2024 Jijini Dodoma amekutana na Mkurugenzi Mtendaji wa COSTECH Dr Amos Nungu na kujadili juu ya maandalizi ya Kongamano la tisa la Kitaifa la Sayansi, Teknolojia na Ubunifu (STICE).
THE STIPENDIUM HUNGARICUM SCHOLARSHIP AVAILABLE FOR THE ACADEMIC YEAR 2025/2026
1.0 Call for Application
Dkt. Charles Wilson Mahera akikagua mabanda kwenye ufunguzi wa Mkutano wa Wadau wanaotekeleza Afua za vijana Balehe Nchini
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia anayeshughulikia masuala ya Elimu Dkt. Charles Wilson Mahera akikagua mabanda kwenye ufunguzi wa Mkutano wa Wadau wanaotekeleza Afua za vijana Balehe Nchini.

Mkutano huu unalenga kujadili utekelezaji na hamasa katika kuwekeza afua hizo umeanza hii leo Octoba, 31 na utatamatika tarehe 1, Novemba, 2024. Mkutano huo unafanyika katika Viwanja vya Hotel ya St. Gaspar

