TUNARIDHISHWA NA HATUA YA UJENZI SEKONDARI 100 ZA AMALI NA VYUO VYA UFUNDI - MHE BITEKO
MAHITAJI YA UANZISHWAJI MKONDO WA AMALI KWA FANI 9
SHILINGI BILIONI 4 KUJENGA CHUO CHA VETA TARIME - MHE. KIPANGA
Shule 100 za Mafunzo ya Amali Kujengwa Nchini - Prof Mkenda
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda amesema Serikali inajenga Shule 100 za Mafunzo ya Amali Uhandisi, ili kuwawezesha Vijana kupata ujuzi na kuwa mahiri.

Prof. Mkenda amesema hayo Oktoba 01, 2024 Mkoani Tanga wakati wa uzinduzi wa Shule ya Sekondari ya Miles & Kimberly White, ambapo amesema Wizara inaendelea kusimamia mageuzi ya Elimu, ikiwemo kuweka msukumo wa mafunzo ya amali yanayojikita kwenye ujuzi zaidi.
KAMPASI YA CHUO KIKUU MZUMBE KUJENGWA TANGA
Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Omary Kipanga ameahidi kushughulikia changamoto za kielimu zinazoikabili Wilaya ya Muheza Mkoani Tanga ikiwemo kuanzisha Shule za kidato cha tano na sita na kujenga tawi la Chuo Kikuu cha Mzumbe Mkoani Tanga.
Karibu katika Mfumo mpya wa uanzishaji na usajili wa Shule (SAS)
Karibu katika Mfumo mpya wa uanzishaji na usajili wa Shule (SAS). Sajili kupitia sas.moe.go.tz
Mfumo huu unanza rasmi kutumika tarehe 01 Oktoba, 2024.
Mfumo ni Maalum kwa Wadau wote wanaohitaji kuanzisha na kusajili Shule za Awali, Awali na Msingi, Sekondari na Vyuo vya Ualimu.
Pia mfumo unatumika kufanya maboresho au mabadiliko ya taarifa za shule au Chuo.
Kwa msaada na mwongozo zaidi tupigie 0784263198 au 0717915175
Au unaweza kuwasiliana nasi kupitia Kituo cha Huduma kwa Wateja kwa namba 0262160270 au 0737962765

