ELIMU YA WATU WAZIMA INACHOCHEA MAENDELEO YA WATANZANIA 

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Carolyne Nombo amesema Elimu ya Watu Wazima na Elimu Nje ya Mfumo Rasmi ina mchango mkubwa katika kuwezesha wananchi kupata maarifa, ujuzi na mielekeo stahiki kwa maendeleo endelevu.



Prof. Nombo ametoa kauli hiyo Oktoba 10, 2024 Mkoani Tabora akifungua Kongamano la Wadau wa elimu ambapo amesema Serikali inatambua kinadharia na vitendo umuhimu wa Elimu ya Watu Wazima na Elimu Nje ya Mfumo Rasmi.

Swahili

Pages

Subscribe to Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia RSS