WIZARA YA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA KINARA USIMAMIZI BORA WA RASILIMALIWATU

Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imeibuka Mshindi wa Kwanza katika kundi la Wizara kwenye usimamizi bora wa Rasilimaliwatu.

Tuzo hiyo imetolewa na Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora katika Mkutano wa Wakuu wa Idara za Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma uliofanyika Jijini Dodoma.

Swahili

Darasa la watoto wadogo katika Chuo cha Maendeleo ya Wananchi (FDC) Kasulu

Katika Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi vyote 54 Serikali kwa kushirikiana na Wadau imejenga madarasa ya watoto wadogo kwa malengo makuu mawili ikiwemo mafunzo pamoja na kutoa huduma ya malezi kwa watoto wa wanafunzi waliorejea na kuendelea na masomo baada ya kujifungua na kuacha shule.



Zaidi ya wanafunzi 1,138 wanaendelea na elimu ya sekondari katika vyuo hivyo kupitia mpango wa Elimu Haina Mwisho ambapo pia wanasoma masomo ya fani za amali wanazochagua

Swahili

Pages

Subscribe to Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia RSS