Prof. Daniel Mushi amekagua ujenzi wa miundombinu katika Chuo Kikuu cha Elimu Mkwawa (MUCE)

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Daniel Mushi Januari 11, 2025 amekagua ujenzi wa miundombinu mbalimbali katika Chuo Kikuu cha Elimu Mkwawa (MUCE) inayotekelezwa kupitia mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi (HEET).



Majengo yaliyokaguliwa ni pamoja na Jengo la Sayansi, Jengo la Multimedia na Elimu Maalum, jengo la Maabara ya Fizikia, maktaba na hosteli ambapo ujenzi umefikia asilimia 12.

Swahili

Viongozi wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia wakizungumza na Waandishi wa habari kuhusu uzinduzi wa Sera ya Elimu na Mafunzo 2014, Toleo la 2023

Viongozi wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia leo Januari 10, 2025 jijini Dodoma wakizungumza na Waandishi wa habari kuhusu uzinduzi wa Sera ya Elimu na Mafunzo 2014, Toleo la 2023 tarehe 31 Januari 2025 katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Convention Centre jijini Dodoma

Swahili

SERA MPYA YA ELIMU IMEZINGATIA MATUMIZI YA KEKNOLOJIA KATIKA UJIFUNZAJI PROF. NOMBO

Katibu Mkuu, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Carolyne Nombo amesema Sera ya Elimu na Mafunzo ya Mwaka 2014, Toleo la 2023, imezingatia na kusisitiza matumizi ya teknolojia za kidijitali katika sekta ya elimu ili kurahisisha ujifunzaji na ufundishaji.



Aidha, pamoja na masuala mengine, amesisitiza dhamira ya Serikali katika kujenga uwezo na kuzalisha walimu mahiri kwenye matumizi ya teknolojia za kidijitali.

Swahili

Prof. Carolyne Nombo amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID)

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Carolyne Nombo amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID) Nchini Dkt. Thomas LeBlanc ambapo wamejadiliana juu ya masuala mbalimbali ya elimu.

Swahili

Pages

Subscribe to Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia RSS