SERIKALI KUENDELEA KUANDAA WATALAAMU WA AKILIUNDE NA SAYANSI SHIRIKISHI
Serikali imejipanga kuongeza wataalam katika eneo la teknolojia ya Habari na Mawasiliano pamoja na Akili unde kwa kusomesha watanzania nje ya nchi na kuongeza miundombinu na vifaa vya kisasa vya kufundishia na kujifunzia katika eneo hilo.
UJENZI WA KAMPASI YA MZUMBE MKOANI TANGA WAFIKIA ASILIMIA 80
KAMATI YAKOSHWA UTEKELEZAJI UJENZI KAMPASI YA MZUMBE - TANGA
MKINGA NA MAONO YA GOMBERO KUWA MJI WA KIELIMU
DUCE YAANZA KUTOA SHAHADA YA UZAMIVU KATIKA LUGHA ZA KIAFRIKA
Chuo Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam kwa mara ya kwanza mwaka huu kinaanza kutoa Shahada ya Uzamivu katika Lugha za Kiafrika ( PhD in African Languages)

Hayo yamesemwa Machi 14, 2026 jijini Dar es Salaam na Rasi wa Chuo hicho Prof. Stephen Maluka wakati wa ziara ya Kamati ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo.
KAMATI YA BUNGE YAPONGEZA MAZINGIRA RAFIKI KWA WANAFUNZI WENYE MAHITAJI MAALUM DUCE
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo wamekipongeza Chuo Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam kwa kuweka mazingira rafiki kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum kusoma bila changamoto yoyote.
HISABATI NI MSINGI WA MAENDELEO YA SAYANSI NA TEKNOLOJIA
Serikali imesisitiza umuhimu wa kuimarisha ufundishaji na ujifunzaji wa somo la Hisabati nchini, ikieleza kuwa somo hilo ni msingi wa maendeleo ya sayansi, teknolojia na uchumi wa taifa.
WAZIRI MKUU AWEKA JIWE LA MSINGI KAMPASI YA MIZENGO PINDA – SUA
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, ameweka jiwe la msingi la ujenzi wa majengo mapya ya Kampasi ya Mizengo Pinda ya Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), iliyopo katika Halmashauri ya Mpimbwe, Wilaya ya Mlele mkoani Katavi. Kampasi hii imekuwa chachu ya maendeleo ya elimu na fursa kwa vijana wa eneo hili na taifa kwa ujumla tangu kuanzishwa kwake mwaka 2019.
SUA YAONGEZA FURSA YA ELIMU YA JUU KATAVI
Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Wanu Hafadh Ameir amesema kuwa ujenzi wa majengo mapya katika Kampasi ya Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), Kampasi ya Mizengo Pinda, mkoani Katavi ni hatua ya kimkakati katika kuongeza fursa za elimu ya juu na kuimarisha utafiti wa kilimo nchini.

