SKAUTI INADUMISHA MSHIKAMANO NA USTAWI WA VIJANA KITAIFA - WAZIRI MKENDA

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, ambaye pia ni rais wa Chama cha Skauti Tanzania Prof. Adolf Mkenda amesema kuwa chama hicho kinasaidia kujenga mshikamano wa vijana, kukuza maadili na uzalendo kwa vijana Nchini.



Waziri Mkenda ameeleza hayo Januari 9, 2026 Mkoani Pwani akifungua Mkutano wa 7 wa chama hicho, akisisitiza kuwa, Wizara itaendelea kuimarisha uskauti katika taasisi za elimu ili kiendelee kujenga ustawi wa nchi.

Swahili

SERIKALI YAENDELEA KUGHARIMIA ELIMU YA UFUNDI, DIT SONGWE YATAJWA KUWA KICHOCHEO CHA MAENDELEO

Serikali ya Awamu ya Sita imeendelea kuwekeza kwa kiasi kikubwa katika elimu ya ufundi nchini ikiwemo kugharimia chakula na mafunzo kwa vitendo viwandani kwa maelfu ya wanafunzi, ili kuzalisha rasilimaliwatu yenye ujuzi unaokidhi mahitaji ya soko la ajira na kuchochea maendeleo ya Taifa.

Swahili

MAGEUZI YA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA KUJENGA UCHUMI IMARA NA ENDELEVU - MHE. SAMIA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema kuwa Serikali imedhamiria kufanya mageuzi ya elimu, sayansi, utafiti na ubunifu ili kujenga uchumi imara na endelevu.



Mhe. Samia amesema hayo Januari 8, 2026 baada ya kuzindua Jengo la Taaluma na Utawala la Taasisi ya Sayansi za Bahari Zanzibar Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM - MSI). Amesisitiza kuwa Taasisi hiyo, ni mdau muhimu kwa Serikali katika kujenga uchumi shindani na shirikishi.

Swahili

Pages

Subscribe to Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia RSS