Wizara na Wamiliki wa Shule Zisizo za Serikali Wakutana Kujadili Changamoto katika Elimu

Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imefanya mkutano na Wamiliki wa Shule zisizo za Serikali kwa lengo la kusikiliza na kujadiliana kwa pamoja changamoto zilizopo katika sekta hiyo.

Akizungumza Oktoba 10, 2023 jijini Dodoma, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda amesema mkutano huo ni wa Kihistoria kwani kwa mara ya kwanza unafanyika ikiwa ni ushirikishwaji wa Sekta Binafsi na unalenga kusikiliza changamoto katika uwekezaji, uendeshaji wa shule na kuona namna ya kusaidia kuzitatua na kuweka mikakati ya pamoja.

Swahili

Hongera Mhe. Samia Suhluhu Hassan

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan ametunukiwa Shahada ya Heshima ya Udaktari wa Falsafa (Doctorate Honoris Causa) na Chuo Kikuu cha Jawaharlal Nehru kwenye hafla iliyofanyika New Delhi nchini India tarehe 10 Oktoba, 2023.

Rais Samia ni Mwanamke wa Kwanza kutunukiwa Shahada hiyo ya Heshima na Chuo hicho nchini India. Ni Viongozi wawili tu ambao wametunukiwa Shahada hiyo ya Heshima akiwemo Rais wa Urusi Mhe. Vladmir Putin pamoja na Aliyekuwa Waziri Mkuu wa Japan Hayati Shinzo Abe.

Swahili

Vyuo Vikuu Vyatakiwa Kufanya Tafiti zenye Tija Kuchochea Ushindani katika Ugunduzi

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda amesema Vyuo vikuu havipimwi kwa wingi wa wanafunzi na mapato badala yake tafiti inazofanya zenye kuleta gunduzi, kukuza maarifa na ujuzi katika jamii

Prof. Mkenda amesema hayo jijini Dodoma wakati akizindua Baraza jipya la Chuo Kikuu Huria cha Tanzania na kutoa wito kwa Vyuo vikuu kuzingatia ufanyaji wa tafiti zenye tija nchini ili kuchochea ushindani katika gunduzi mbalimbali ndani na nje ya nchi.

Swahili

Pages

Subscribe to Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia RSS