Prof. Nombo Akutana na Kansela Mkuu wa Ushirikiano na Maendeleo kutoka ubalozi wa Canada hapa nchini

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Nombo leo Oktoba 12, 2023 jijini Dar es Salaam amekutana na kufanya mazungumzo na Bi. Helen Fytche, Kansela Mkuu wa Ushirikiano na Maendeleo kutoka ubalozi wa Canada hapa nchini ambae ameambatana na Bi. Rasmata Barry, muambata wa masuala ya maendeleo ya elimu.

Mazungumzo yamelenga kuimarisha ushirikiano baina ya Tanzania na Canada na kuona namna ya kuanzisha maeneo mapya ya ushirikiano katika Sekta ya elimu.

Swahili

Siku ya Kimataifa ya Mtoto wa Kike, Tunasheherekea Mafanikio yao Kwenye Elimu - Prof. Mkenda

Tanzania inajivunia kutekeleza kwa vitendo hatua za kuhakikisha mtoto wa kike anapata haki katika ngazi zote za elimu.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof.Adolf Mkenda amesema hayo Oktoba 11, 2023 jijini Dodoma katika maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Mtoto wa Kike yaliyojikita kusherehekea mafanikio ya mtoto wa kike kwenye elimu na kufanyika jijini Dodoma

Swahili

Huduma Bora kwa Wanafunzi ni Haki yao Prof. Mdoe

Na Mwandishi Wetu, Bagamoyo

Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. James Mdoe amewataka maafisa wanaosimamia madawati ya mikopo katika taasisi mbalimbali za elimu ya juu nchini kutoa huduma bora kwa wanafunzi.

Prof. Mdoe ametoa wito huo leo Oktoba 11, 2023 wakati akifungua kikao kazi cha siku tatu kati ya Menejimenti ya Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) na maafisa mikopo kutoka taasisi 80 zenye wanafunzi wanufaika wa mikopo ya elimu ya juu.

Swahili

Dkt. Rwezimula Ahimiza Ushiriki Katika Maadhimisho ya Kitaifa Juma la Elimu ya Watu Wazima

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Franklin Rwezimula leo Oktoba 11, 2023 amewahimiza Wananchi kutoka mikoa yote kutumia vema Maadhimisho ya Kitaifa ya Juma la Elimu ya Watu Wazima, kuona mafanikio ya program mbalimbali za Kielimu zinazotplewa na Taadidi hiyo pamoja na Taasisi za Elimu ya Juu, Vyuo vya Kati na vya Ufundi.

Swahili

HONGERA WyEST

Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imekuwa Mshindi wa kwanza katika Tuzo zilizotolewa na Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala bora leo tarehe 11/10/202023 katika Mkutano wa wakuu wa Idara na usimamizi wa Rasilimaliwatu katika utumishi wa umma kwa kufanya vizuri kwenye Usimamizi bora wa Rasilimaliwatu kwenye kundi la Wizara

 

Swahili

Pages

Subscribe to Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia RSS