Prof. Mkenda atazindua ufadhili kwa Wanafunzi wa Kike wanaosoma programu za Uhandisi katika sekta ya usafirishaji na kuweka jiwe la msingi
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda leo Oktoba 28, 2023 atazindua ufadhili (Scholarship) kwa Wanafunzi wa Kike wanaosoma programu za Uhandisi katika sekta ya usafirishaji pamoja na kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa majengo matano ya Chuo cha Taifa cha Usafirishaji yanayofadhiliwa na Benki ya Dunia kupitia Mradi wa Kujenga Ujuzi na Ushirikiano wa Kikanda wa Afrika Mashariki (EASTRIP).

