Kipanga Kazini VETA Arumeru
Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Omari Kipanga amewahimiza wasimamizi wa mradi wa Ujenzi wa VETA ya Wilaya ya Arumeru kukamilisha hatua ya kwanza ya kujenga Msingi kwa wakati na kuwataka kufanya marekebisho katika maeneo yenye Changamoto zilizobainika.
Mhe. Kipanga ametoa rai hiyo Desemba 19, 2023, akiwa katika ziara ya Kukagua na kufanya tathmini ya ujenzi wa VETA hiyo ikiwa ni moja ya VETA 63 zinazojengwa na Serikali nchini.



