Kipanga Kazini VETA Arumeru

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Omari Kipanga amewahimiza wasimamizi wa mradi wa Ujenzi wa VETA ya Wilaya ya Arumeru kukamilisha hatua ya kwanza ya kujenga Msingi kwa wakati na kuwataka kufanya marekebisho katika maeneo yenye Changamoto zilizobainika.

Mhe. Kipanga ametoa rai hiyo Desemba 19, 2023, akiwa katika ziara ya Kukagua na kufanya tathmini ya ujenzi wa VETA hiyo ikiwa ni moja ya VETA 63 zinazojengwa na Serikali nchini.

Swahili

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe Hemed Suleiman Abdulla amefungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama cha Skauti Tanzania

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe Hemed Suleiman Abdulla Leo Disemba 19, 2023 amefungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama cha Skauti Tanzania uliofanyika Zanzibar Chini ya uenyekiti wa rais wa chama hicho Prof Adolf Mkenda ambae ni Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia ambapo amewataka wajumbe wa mkutano huo kutoa michango na uzoefu wao ili kuweka na mikakati imara ambayo itasaidia kuimarisha uskauti Tanzania.

Swahili

Mhe. Omari Kipanga Kukutana Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Emanuela Kaganda

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Omari Kipanga leo Desemba 19, 2023 amefika Ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Arumeru na Kukutana Mkuu wa Wilaya hiyo Emanuela Kaganda kabla ya kuelekea Kukagua Shughuli za ujenzi wa VETA ya Wilayani hiyo.



Pia Naibu Waziri huyo alipata wasaa wa kusikiliza na kujibu hoja za baadhi ya wananchi waliofika kwenye ofisi ya mkuu wa wilaya ya Arumeru kuhusu sekta ya elimu.

Swahili

Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Dar es Salaam imetoa Tuzo Maalum kwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutambua mchango wake katika Sekta ya Elimu

Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Dar es Salaam imetoa Tuzo Maalum kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kutambua mchango wake katika kuleta mageuzi katika sekta ya elimu kwa kuelekeza kufanyika kwa Mapitio ya Sera na Mitaala ili iweze kulenga kutoa ujuzi.

Tuzo hiyo imepokelewa na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda kwa niaba ya Mhe. Rais.

Swahili

Utekelezaji wa Sera ya Elimu na Mafunzo ya Mwaka 2014 Toleo la 2023 pamoja na Mitaala mipya kwa elimu ya Sekondari itaanza mwakani kwa mkondo wa elimu ya Amali.

Serikali imesema utekelezaji wa Sera ya Elimu na Mafunzo ya Mwaka 2014 Toleo la 2023 pamoja na Mitaala mipya kwa elimu ya Sekondari itaanza mwakani kwa mkondo wa elimu ya Amali.

Akizungumza Disemba 18, 2023 Jijini Dar ea Salaam wakati akiongea na Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Dar es Salaam, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda amesema mageuzi ya elimu yatatekelezwa kwa awamu ambapo madarasa yatakayoanza na mitaala mipya ni awali, la kwanza na la tatu kwa shule za msingi na kidato cha kwanza shule za mkondo wa Amali pekee.

Swahili

Pages

Subscribe to Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia RSS