Prof. Mkenda ameiambia Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Elimu kuwa watoto wote waliotoka nje ya mfumo rasmi wa elimu kwa sababu zozote zile wanarudi shule

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda ameiambia Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Elimu, Utamaduni na Michezo kuwa Serikali itaendelea kuhakikisha watoto wote waliotoka nje ya mfumo rasmi wa elimu kwa sababu zozote zile wanarudi shule ili kupata elimu na ujuzi na kutimiza ndoto zao za kuwaletea maendeleo binafsi na ya Taifa.

Swahili

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu wakielezwa namna Taasisi ya Elimu ya Watu wazima inavyotekeleza majukumu yake

Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo wakielezwa namna Taasisi ya Elimu ya Watu wazima inavyotekeleza majukumu yake .

Katika ziara hiyo Kamati ilijionea vitabu mbalimbali vinavyotumiwa na Taasisi hiyo katika mchakato wa kufundishia na kujifunzia.

Swahili

Prof. Adolf Mkenda akizungumza na baadhi ya wanafunzi waliorejea shuleni baada ya kukatisha masomo ya Sekondari kutokana na Changamoto Mbalimbali

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda akizungumza na baadhi ya wanafunzi waliorejea shuleni baada ya kukatisha masomo ya Sekondari kutokana na changamoto mbalimbali. Wanafunzi hao wanaso katikaa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima

Swahili

Prof. Adolf Mkenda amekutana na kufanya mazungumzo na Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB Bi. Ruth Zaipuna

Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda tarehe 18,01,2024 amekutana na kufanya mazungumzo na Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB Bi. Ruth Zaipuna alipomtembelea katika Ofisi za Wizara, Dodoma.



Viongozi hao wamejadili mikakati ya kuendeleza ushirikiano na ufadhili wa Benki katika Miradi mbalimbali ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ikiwemo Wiki ya Ubunifu, uimarishaji Shule za Sekondari za Ufundi na Uandishi Bunifu.

Swahili

Prof. Adolf Mkenda amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkaazi wa Shirika la Kimataifa la Misaada la Watu wa Marekani (USAID)

Leo Januari 18, 2024 Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Prof. Adolf Mkenda amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkaazi wa Shirika la Kimataifa la Misaada la Watu wa Marekani (USAID), Bw. Craig Hart.



Kikao hicho kimelenga kujadili ushirikiano katika kuimarisha sekta ya Elimu , utekelezaji wa Sera ya Elimu na Mafunzo na Mitaala Mipya pamoja na kushirikiana katika kufanya mapitio ya programu na miradi wanazotekeleza.

Swahili

Prof. Nombo akifafanua jambo katika kikao na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC)

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof Caloryne Nombo akifafanua jambo katika kikao na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) chini ya Mwenyekiti wake, Mhe Naghenjwa Kaboyoka jijini Dodoma.

Kamati hiyo imepitia na kuchambua taarifa ya ukaguzi wa kiufundi kuhusu ujenzi wa Shule za Sekondari kupitia mradi wa kuboresha Elimu ya Sekondari (SEQUIP) unaotekelezwa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na Ofisi ya Rais TAMISEMI kikao hicho pia kimehudhuriwa na Katibu Mkuu OR- TAMISEMI anaeshughulikia Miundo Mbinu Mhandisi Rogatus Mativila.

Swahili

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu imeendelea na vikao vya Kupitia taarifa za Utekelezaji wa Majukumu ya Wizara na Taasisi zake

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo Chini ya Mwenyekiti wake Mhe. Husna Sekiboko imeendelea na vikao vya Kupitia taarifa za Utekelezaji wa Majukumu ya Wizara na Taasisi zake.

Leo ilikua ni zamu ya Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu ambapo imewasilisha taarifa ya Utendaji ya Bodi kwa Mwaka wa fedha 2023/24.

Swahili

Pages

Subscribe to Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia RSS