Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu imekutana na Wizara ya Elimu kujadili utekelezaji wa majukumu mbalimbali ya Elimu
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo imekutana na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na kujadili utekelezaji wa majukumu ya Elimu ya Ualimu na maendeleo ya elimu ya ufundi na mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) ambapo kamati hiyo imeridhishwa na utekelezaji na mipango ya kuimarisha ngazi hizo za Elimu.


