Wizara 5 Kujadiliana Mwarobaini Upungufu wa Wataaluma Vyuo vya Afya
Na WyEST
Dodoma
Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknojia, Wizara ya Fedha, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Uwekezaji wakutana pamoja kujadili namna ya kutatua changamoto ya upungufu wa Wanataaluma katika Vyuo Vikuu na Kati vinavyotoa Elimu ya Afya na Tiba nchini.
Kikao hicho kilichofanyika Januari 23, 2024 Jijini Dodoma kimeongozwa na Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. James Mdoe pia kimejadili changamoto ya miundombinu na vifaa vya kufundishia na kujifunzia katika vyuo hivyo.





