Watumishi Watakiwa Kutumia Lugha Nzuri kwa Walimu

Dr. Charles Msonde, Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI (ELIMU), ameanza rasmi ziara yake ya kikazi Mkoa wa Dodoma Leo Mei 27, 2024 kwa kuzungumza na Walimu wa shule za Msingi na Sekondari za Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwenye ukumbi wa Shule ya Msingi St. Gasper iliyopo Miyuji.

Katika kikao hicho, Dr. Msonde ametatua changamoto mbalimbali zinazowakabili walimu kwa ujumla ikiwa ni pamoja na upandishwaji wa madaraja, madai ya malipo, likizo, uhamisho, maslahi n.k

Swahili

Bunge la Tanzania linatamani kuona Bunifu zinazoibuliwa zinaboreshwa ili zilete Tija na kutatua Chamamoto mbalimbali za Kijamii - Mhe. Husna Sekiboko

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge Elimu, Michezo na Utamaduni Mhe. Husna Sekiboko amesema Bunge la Tanzania linatamani kuona bunifu zinazoibuliwa zinaboreshwa ili zilete tija na kutatua chamamoto mbalimbali za kijamii.

Swahili

Prof. Adolf Mkenda amefika Jijini Tanga kwa ajili ya Uzinduzi wa Maadhimisho ya Kitaifa ya Wiki ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda tayari amefika Jijini Tanga kwa ajili ya Uzinduzi wa Maadhimisho ya Kitaifa ya Wiki ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu



Prof. Mkenda leo Mei 27, 2024 amewasili katika Ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Balozi Dkt. Batilda Burian akiwa ameongozana na Katibu Mkuu Prof. Carolyne Nombo pamoja na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Michezo na Utamaduni Mhe. Husna Sekiboko (Mb).

Swahili

Serikali inaendelea kuwekeza miundombinu mbalimbali katika sekta ya Elimu ikiwemo katika Vyuo vya Elimu ya Juu - Prof. Nombo

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Carolyne Nombo amesema Serikali inaendelea kuwekeza miundombinu mbalimbali katika sekta ya Elimu ikiwemo katika Vyuo vya elimu ya juu ili Vijana wa Kitanzania waweze kupata Elimu bora itakayowawezesha kushiriki katika maendeleo ya Taifa.

Prof. Nombo ameeleza hayo Mei 27, 2024 Jijini Tanga wakati akizungumza na Waandishi wa habari juu ya Maadhimisho ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu yanayofanyika katika viwanja vya shule ya Sekondari Popatlal.

Swahili

Maadhimisho ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu chachu ya Maendeleo Sekta za Uzalishaji

Mkuu wa Wilaya ya Tanga Mhe. James Kaji amesema Wiki ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu italeta chachu ya maendeleo ya Viwanda na uchumi kwa mkoa wa Tanga na Tanzania kwa ujumla.

Mhe. Kaji amesema hayo Mei 26, 2025 wakati akizungumza na Waandishi wa Habari katika Viwanja vya Shule ya Sekondari Popatlal ambapo amesisitiza Wanatanga kutumia fursa hiyo kujifunza masuala mbalimbali ikiwemo Teknolojia na ubunifu.

Swahili

Pages

Subscribe to Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia RSS