Watumishi Watakiwa Kutumia Lugha Nzuri kwa Walimu
Dr. Charles Msonde, Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI (ELIMU), ameanza rasmi ziara yake ya kikazi Mkoa wa Dodoma Leo Mei 27, 2024 kwa kuzungumza na Walimu wa shule za Msingi na Sekondari za Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwenye ukumbi wa Shule ya Msingi St. Gasper iliyopo Miyuji.
Katika kikao hicho, Dr. Msonde ametatua changamoto mbalimbali zinazowakabili walimu kwa ujumla ikiwa ni pamoja na upandishwaji wa madaraja, madai ya malipo, likizo, uhamisho, maslahi n.k


