Prof. Carolyne Nombo amekutana na Balozi wa Poland Nchini Tanzania kujadili kuhusu kukuza ushirikiano katika sekta ya Elimu

Karibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Carolyne Nombo Mei 17 2024 amekutana na Balozi wa Poland Nchini Tanzania Mhe. Krzystof Buzalski ambapo wamezungumzia kuhusu kuendelea kukuza ushirikiano kati ya nchi hizo mbili katika sekta ya Elimu.

Swahili

Prof. Carolyne Nombo amekutana na Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa kujadiliana na masuala mbalimbali ya Elimu

Karibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Carolyne Nombo Mei 16, 2024 amekutana na Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa Canada Mhe. Ahmed Hussen kujadiliana na masuala mbalimbali ya Elimu.



Prof. Nombo ameishukuru Serikali ya Nchi hiyo kuendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania kupitia miradi mbalimbali ikiwemo Mradi wa Kuendeleza Elimu ya Ualimu (TESP).

Swahili

Kongole Mhe. Dkt. Mpango

Picha mbalimbali za Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akinunua vitabu katika maduka jijini Dar es salaam ikiwemo Duka la Mkuki na Nyota na Pauline’s Bookshop.



Makamu wa Rais hutumia muda wa mapumziko katika kujisomea vitabu kwa lengo la kuongeza maarifa katika njanja mbalimbali za uchumi, utawala, dini, siasa, kilimo na ufugaji vilivyoandikwa na waandishi wa ndani na nje ya nchi.

Swahili

Prof. Nombo Aridhishwa na Kazi - Ujenzi wa VETA Wilaya ya Muheza

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Carolyne Nombo ameridhishwa na kazi inayoendelea ya ujenzi wa Chuo cha Ufundi VETA cha Wilaya ya Muheza mkoani Tanga.



Prof. Nombo akikagua ujenzi wa Chuo hicho Mei 15, 2024 amemtaka Mkandarasi kuongeza kasi ya ujenzi na kushirikiana kikamilifu na Msimamizi wa mradi huo ili kukamilisha kwa wakati.

Swahili

Pages

Subscribe to Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia RSS