Walimu ni Nguzo ya Elimu Nchini - Prof. Nombo
Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Carolyne Nombo amewataka Wakufunzi katika Chuo cha Ualimu tarajali Korogwe jijini Tanga kufahamu mwelekeo wa elimu, na kuhakikisha wanawajibika kikamilifu katika kutekeleza mabadiliko ya Elimu yanayolenga kuimarisha ufundishaji kidijitali.

Nombo ametoa rai hiyo Mei 29, 1024 jijini Tanga wakati akizungumza na Wakufunzi na Wafanyakazi Mwega wa Chuo hicho kuhusu masuala mbalimbali ya Elimu.


