ENABEL Wapokea Tuzo ya Shukrani Kuendeleza Ushirikiano Utekelezaji Miradi ya Elimu

Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia leo Julai 03, 2024 inetoa Tuzo ya Shukrani kwa Shirika la Maendeleo la Ubelgiji (ENABEL) kwa kudhamini Wiki ya Elimu Ujuzi na Ubunifu Mwaka 2024 iliyofanyika Mkoani Tanga Mwezi Mei.



Tuzo hiyo imekabidhiwa Jijini Dar es Salaam na Katibu Mkuu Profesa Carolyne Nombo ambae amewashukuru kwa ufadhili huo pamoja na ufadhili miradi ya elimu Mkoani Kigoma.

Swahili

Katibu Mkuu Kiongozi Mstaafu kufunga Mafunzo kwa Viongozi wa Menejimenti ya WyEST

Katibu Mkuu Kiongozi Mstaafu Philemon Luhanjo kufunga Mafunzo kwa Viongozi wa Menejimenti ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia.



Mafunzo hayo ya siku tatu yanahutimishwa leo 03.07.2024 Jijini Dar es Salaam ambapo kabla ya kufunga mafunzo hayo Katibu Mkuu Kiongozi alifanya mazungumzo na Katibu Mkuu Wizara ya elimu sayansi na Teknolojia Prof Carolyne Nombo pamoja na Dkt Rwezimula Naibu Katibu Mkuu

Swahili

Mafunzo kwa viongozi Yanaendelea

Mafunzo kwa Menejimenti ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia yanaendelea ikiwa ni leo Julai 02, 2024 yameingai siku ya pili ambapo Viongozi hao wanawezeshwa juu ya mbinu na mikakati mbalimbali ya uongozi ili kuongeza tija na Ufanisi katika utendaji kazi.



Mchezo wa Blind Fold unaohusisha kuundwa kwa makundi mbalimbali umesaidia kuonesha aina za uongozi ( leadership styles )

Swahili

Mafunzo kwa Viongozi

Mafunzo ya Menejimenti ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia yanaendelea ikiwa ni siku ya pili ambapo Viongozi wanapata katika mbinu na mikakati mbalimbali ya uongozi ili kuongeza tija katika utendaji na kuleta matokeo chanya.

Swahili

Serikali ya Canada kuendeleza ushirikiano katka elimu

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknoljia Prof. Carolyne Nombo alikutana na Mkuu wa Ushirikiano katika Masuala ya Elimu kutoka Serikali ya Canada Bi Hellen Fytche aliyefika Ofisini kwake kumuaga baada ya kumaliza muda wake wa kazi nchini.



Mkutano huo umefanyika Juni 27, 2024 Jijini Dar es Salaam ambapo Katibu Mkuu alimshukuru Bi Fytche kwa mchango wake katika sekta ya elimu hasusan katika kuimarisha Elimu ya Ualimu.

Swahili

Pages

Subscribe to Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia RSS