Michezo Itasaidia Vijana Kujiepusha na Matendo Maovu

Imeelezwa serikali kuwa itahakikisha michezo inaendelezwa shuleni kwa sababu inasaidia vijana kujiepusha na matendo yasiyofaa.



Hayo yamesemwa leo Julai 20, 2024 na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda wakati wa ufunguzi wa mashindano ya mpira wa miguu ya Wazazi Dar es salaam Super Cup yaliyoanza kutimua vumbi rasmi katika viwanja vya Bandari Jijini Dar es salaam,

Swahili

Prof. Carolyne Nombo na Wataalamu wa Elimu Wameshiri Kikao cha Pamoja na Wizara Ya ElimuMsingi ya Afrika Kusini

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo na wataalamu wa elimu kutoka Tanzania Bara na Zanzibar wameshiriki kikao cha pamoja na Wizara Ya ElimuMsingi ya Afrika Kusini ambapo ameipongeza Wizara hiyo kwa jitihada kubwa wanazozifanya katika sekta ya elimu.

Swahili

Kuweni Wabunifu Kutekeleza Majukumu ili kuwapatia Vijana wa Mkoa wa Njombe Elimu na Ujuzi

Watumishi wa Chuo cha Wananchi Njombe (FDC) wametakiwa kiwa wabunifu katika kutekeleza majukumu ili kuwapatia vijana wa Mkoa wa Njombe elimu na ujuzi utakaowasaidia kujianiri ama kuajiriwa.



Wito huo umetolewa Julai 19, 2024 Mkoani Njombe na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Franklin Rwezamula wakati alipofika mkoani humo kufatilia mradi wa ukarabati wa chuo hicho.

Swahili

Prof. Adolf Mkenda amefanya ziara katika Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Dar es Salaam Kampasi ya Myunga Songwe

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda amefanya ziara katika Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Dar es Salaam Kampasi ya Myunga Songwe



Prof. Mkenda amefanya ziara hiyo na kukagua miundombinu ya kampasi hiyo akiwa ameongozana na Mbunge wa Jimbo la Momba Mhe. Condester Sichalwe pamoja na Naibu Katibu Mkuu Dkt. Franklin Rwezamula.

Swahili

Lugha ya Kiswahili Yaendelea Kuchanja Mbuga

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknolojia Prof. Carolyne Nombo anaendelea na ziara ya mafunzo nchini Afrika Kusini akiwa anaongoza timu ya wataalam kutoka Tanzania Bara na Zanzibar wanaoshughulika na Sayansi, Teknolojia na ElimuMsingi.



Ziara hiyo pia ni sehemu ya utekelezaji wa hati ya Makubaliano baina ya Tanzania na Afrika Kusini kuhusu kuhusu ElimuMsingi ikiwemo ufundishaji wa Kiswahili katika shule za Afrika Kusini.

Swahili

Pages

Subscribe to Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia RSS