Wizara ya Elimu Kushirikiana na Taasisi ya Vignans ya India eneo la Sayansi, Teknolojia na Utafiti

Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknolojia imetia saini makubaliano ya ushikirikiano na Taasisi ya Utafiti, Sayansi na Teknolojia ya Vignan's kutoka India.



Makubaliano hayo ni katika masuala ya Elimu, Sayansi,Teknolojia na  Utafiti ikiwa ni pamoja na taasisi hiyo kupokea wanafunzi 100 kutoka Tanzania kila mwaka kwa ajili ya kusoma fani za kipaumbele ikiwemo Uhandisi ujenzi, Uhandisi Kilimo, Akili Mnemba, na  Uhandisi wa Umeme kwa gharama nafuu.

Swahili

Rais Samia Amekitaka Chuo Kikuu cha MUST kitakapokamilisha Ujenzi kutoa mafunzo kwa vijana wa Mkoa wa Rukwa

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amekitaka Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya (MUST) kitakapokamilisha ujenzi wa Kampasi ya Rukwa kutoa mafunzo kwa vijana wa mkoa wa Rukwa ya namna ya kutumia rasilimali zinazopatikana katika mkoa huo.

Swahili

Tanzania Imefanya Mageuzi katika Mitaala ambayo ni Utekelezaji wa Maelekezo ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan

Tanzania imefanya mageuzi katika mitaala ambayo ni utekelezaji wa maelekezo ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya kuwa na mitaala inayojikita katika ujuzi.



Hayo yamesemwa na Prof. Carolyne Nombo Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Julai 17, 2024 alipotembelea na kukutana na uongozi wa Chuo cha Ufundi cha Tshwane South nchini Afrika Kusini.

Swahili

Taasisi Zimehimizwa Kujipanga ili kutoa Huduma bora kwa Wananchi

Taasisi zimehimizwa kujipanga ili kutoa huduma bora kwa wananchi na hatimaye kuongeza mchango wa sayansi, teknolojia na ubunfu katika maendeleo ya kiuchumi na kijamii.



Hayo yamesemwa hii leo tarehe 17 Julai 2024 na Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojaia Prof. Carolyne Nombo akiwa nchini Afrika Kusini ambapo amepata nafasi ya kutembelea taasisi ya utafiti wa viwanda ya Afrika Kusini.

Swahili

Zaidi ya Bilioni 15 kutumika katika Ujenzi wa Chuo Kikuu cha MUST Kampasi ya Rukwa

Leo Julai 17,2024 Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ameweka jiwe la msingi katika mradi huo unaojengwa na Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na Benki ya Dunia, Chuo hicho kitakuwa na uwezo wa kuhudumia wanafunzi zaidi ya elfu moja kwa wakati mmoja jambo litakalosaidia vijana wengi kupata Elimu kwa wakati

Swahili

Wananchi Mkoa wa Rukwa Wanaendelea kushuhudia namna WyEST ilivyosogeza Fursa za Elimu katika Mkoa huo.

Leo Julai 17, 2024 wananchi Mkoa wa Rukwa wanaendelea kushuhudia namna Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ilivyosogeza fursa za elimu katika Mkoa huo.



Wananchi wa Mkoa huu wanakwenda kushuhudia Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiweka Jiwe la Msingi la ujenzi wa Kampasi ya Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya (MUST)

Swahili

Prof. Carolyne Nombo Akizungumza na Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara Sayansi na Ubunifu ya Afrika Kusini

Serikali imesema makubaliano ya ushirikiano kati ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na Idara ya Sayansi na Ubunifu ya Afrika Kusini imewezesha kutekelezwa kwa miradi ya pamoja ya kitafiti katika vyuo vikuu na kuendeshwa kwa makongamano ya pamoja ya kujengeana uwezo na mifumo ya udhibiti, kuanzishwa kwa vituo vya teknolojia na uanzishwaji wa vigoda vya OR-TAMBO.

Swahili

Pages

Subscribe to Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia RSS