Prof. Adolf Mkenda ameweka Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Chuo cha Ufundi Arusha Kampasi ya Kikuletwa
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda Julai 30, 2024 ameweka Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Chuo cha Ufundi Arusha Kampasi ya Kikuletwa itakayokuwa Kituo cha Umahiri cha Nishati Jadidifu.

Kampasi hiyo inajengwa katika Wilaya ya Hai Mkoani Kilimanjaro ambapo ikikamilika itakuwa na uwezo wa kuzalisha wataalamu wa Nishati Jadidifu wasiopungua 1,500 kwa Mwaka.





