Waandishi wa Vitabu Waomba Uhamasishaji Usomaji
Mwandishi wa Kitabu cha *Tangled Web* Euanice Urio ameiomba Serikali kusaidia katika mnyororo wa Sekta ya Uandishi wa Vitabu ili kuwezesha upatikanaji wa vitabu na kuhamasisha usomaji nchini

Akizungumza Agosti 02, 2024 Jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa Kitabu chake hicho, Urio amesema kuwa changamoto kubwa katika sekta hiyo ni kuvipeleka sokoni kutokana na watanzania wengi kutokuwa na tabia ya usomaji wa vitabu.








