Shangwe la RC Sendiga akipokea Wanafunzi Shule ya Wasichana Maisaka
Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe. Queen Sendiga ameonesha kufurahishwa kukamilika na kuanza kwa Shule mpya ya Sekondari ya Wasichana Maisaka ya mchepuo wa Sayansi na kutokea Shuleni hapo akiwa amevalia sure ya shule hiyo.

Shule hiyo ni miongoni mwa Shule 26 zilizojengwa na Mradi wa Kuboresha Elimu ya sekondari (SEQUIP) unaotekelezwa na Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia na Ofisi ya Rais TAMISEMI.



