Majaliwa Ahimiza Kuchangamkia Fursa za Mafunzo Fani za Sayansi na Teknolojia

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa amesema, Serikali inaendelea kuweka msisitizo suala la elimu, na katika Mwaka wa fedha 2024/25 imetenga Sh. bilioni 787 kwa ajili ya Mikopo kwa Wanafunzi wa Elimu ya Juu.



Mhe. Majaliwa amesema hayo Agosti 27, 2024 akimwakilisha Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika sherehe za Miaka 50 ya Idara ya Ujenzi ya Chuo cha Sayansi na Teknolojia Karume (KIST) visiwani Zanzibar.

Swahili

Prof. Adolf Mkenda na Prof. Carolyne Nombo waungana na Wazanzibar kusherekea Miaka 50 tangu kuanzishwa kwa KIST

Leo Agosti 27, 2024 Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda na Katibu Mkuu Prof. Carolyne Nombo waungana na Wazanzibar kusherekea Miaka 50 tangu kuanzishwa kwa Idara ya Ujenzi ya Chuo cha Sayansi na Teknolojia Karume (KIST) katika ukumbi wa Golden Tulip Zanzibar.

Swahili

Prof. Adolf Mkenda akizungumza na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Bi. Lela Mohamed

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda akizungumza na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Bi. Lela Mohamed katika Sherehe za kuadhimisha Miaka 50 tangu kuanzishwa kwa Idara ya Ujenzi ya Chuo cha Sayansi na Teknolojia Karume (KIST) Agosti 27, 2024 katika ukumbi wa Golden Tulip Zanzibar.

Swahili

Washiriki mbalimbali wakifuatilia kwa makini zoezi la zawadi kwa Wanafunzi waliofaulu kwa kupata daraja la Kwanza katika Mtihani

Washiriki mbalimbali wakifuatilia kwa makini zoezi la zawadi kwa Wanafunzi waliofaulu kwa kupata daraja la Kwanza katika Mtihani wa Kidato cha Nne mwaka 2023 na Kidato cha Sita 2024 upande wa Unguja.



Halfa ya kuwapongeza Wanafunzi hao imefanyika Agosti 26, 2024 Viwanja vya Mnazi Mmoja Ikulu Zanzibar

Swahili

Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Dkt. Hussein Mwinyi katika hafla ya kuwapongeza Wanafunzi waliopata daraja la Kwanza katika Mtihani yao

Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Dkt. Hussein Mwinyi Agosti 26, 2024 ameambatana na Mama Maryam Mwinyi katika hafla ya kuwapongeza Wanafunzi waliopata daraja la Kwanza katika Mtihani wa Kidato cha Nne mwaka 2023 na Kidato cha Sita 2024 Viwanja vya Mnazi Mmoja Ikulu Zanzibar.

Swahili

Pages

Subscribe to Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia RSS