Mambo Safi Ujenzi wa Shule ya Sekondari Wasichana ya Sayansi Mkoa wa Dar es Salaam
Kamati ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo ikiongozwa na Mwenyekiti Mh. Husna Juma Sekiboko imeridhiswa na ujenzi wa Shule maalum ya wasichana ya Mkoa wa Dar es salaam.

Shule hii ni moja kati ya Shule 26 za Sekondari za wasichana za Sayansi zilizojengwa nchini ili kuongeza fursa za wanafunzi wa kike kusoma masomo ya Sayansi. Shule hizi zinajengwa kupitia Programu ya Uboreshaji wa Elimu ya Sekondari (SEQUIP)





