Prof. Mkenda ameshiriki mazungumzo yaliyoongozwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa GPE Mhe. Dkt. Jakaya Kikwete

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda leo Disemba 2023 jijini Dar es Salaam ameshiriki mazungumzo yaliyoongozwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Ushirikiano wa Elimu Duniani (GPE) Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa GPE Laura Frigenti.

Swahili

Prof. Mkenda akisalimiana na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa GPE Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda akisalimiana na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Ushirikiano wa Elimu Duniani (GPE) Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania baada ya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa GPE Laura Frigenti kuhusu masuala mbalimbali ya elimu.

Swahili

Prof. Mkenda (kulia) akiwa na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha (katikati) pamoja na Mkurugenzi wa Sera na Mipango WyEST

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda (kulia) akiwa na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Dkt. Natu El-Maamry Mwamba (katikati) pamoja na Mkurugenzi wa Sera na Mipango Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Atupele Mwambene.

Swahili

Waziri Mkenda Awataka Wahitimu ADEM kuwa Viongozi wa Mageuzi ya Elimu

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda amesema Serikali inawatarajia Wahitimu katika mafunzo ya elimu kuwa mabalozi wa utekelezaji wa Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014 Toleo la 2023.

Prof. Mkenda ametoa rai hiyo Disemba Mosi, 2023, Bagamoyo Mkoa wa Pwani wakati akizungumza kwenye mahafali ya 31 ya Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (ADEM).

Swahili

Rais Mstaafu Dkt. Kikwete na Afisa Mtendaji Mkuu wa GPE Wakoshwa na Utekelezaji Mradi

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Ushirikiano wa Elimu Duniani (GPE), Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, pamoja na Afisa Mtendaji Mkuu wa GPE, Bibi Laura Frigenti, leo wametembelea na kukagua shule za Msingi ya Maji Matitu iliyoko Mbagala na Mikongeni iliyoko Gongo la Mboto jijini Dar es salaam.

Swahili

Tanzania na Sweden za Saini Mkataba Msaada wa Takriban Bilioni 210 Kuimarisha Kada ya Ualimu kupitia GPE

Tanzania na Sweden, kupitia Taasisi ya Ushirikiano wa Elimu Duniani (GPE) na Shirika la Kimataifa la Ushirikiano wa Kimaendeleo la Sweden (SIDA), zimesaini Mkataba wa msaada wenye thamani ya dola za Marekani milioni 84 sawa na takriban shilingi bilioni 210, kwa ajili ya kuimarisha utekelezaji wa Programu ya kuimarisha Kada ya Ualimu nchini.

Mkataba huo umetiwa saini Jijini Dar es Salaam Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Dkt. Natu El- Maamry Mwamba na Balozi wa Sweden nchini, Mhe. Charlotta Ozaki Marcias.

Swahili

Masomo ya Dini ni ya Kipekee, ni Tofauti na Mitaala ya Masomo Mengine

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda amebainisha kuwa, elimu inayotolewa kupitia masomo ya dini ni tofauti na ile ya masomo mengine kwani elimu hiyo inahusisha masuala ya imani na hugusa zaidi hisia.

Prof. Mkenda alisema hayo Novemba 30, 2023 katika uzinduzi wa Tanzania Islamic Studies Teaching Association (TISTA) pamoja na makabidhiano ya muhtasari na kitabu cha kwanza cha mwanafunzi cha Elimu ya dini ya Kiislamu, tukio lililofanyika katika ukumbi wa Mfalme Mohamed BAKWATA makao makuu Kinondoni Dar es Salaam.

Swahili

Pages

Subscribe to Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia RSS